• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAHIDI KUWA MLEZI BORA KWA MAAFISA USAFIRISHAJI WA SERIKALI

Posted on: March 2nd, 2025

RC MTANDA AAHIDI KUWA MLEZI BORA KWA MAAFISA USAFIRISHAJI WA SERIKALI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefungua kongamano la Maafisa usafirishaji wa Serikali mkoani humo na kuwaahidi kuwa mlezi bora wa chama chao ili kiweze kufikia malengo waliyojiwekea.

Akizungumza nao leo Machi 2, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa Mtanda ambaye ni mlezi wa chama hicho amewakumbusha maafisa hao wa usafirishaji kuendelea na kutimiza wajibu wao wa kulinda usalama barabarani.


"Afisa usafirishaji tambua wewe ni mtu muhimu, tanguliza nidhamu kwa mkuu wako wa kazi, tunza siri na siku zote hakikisha chombo chako ni salama kabla ya kuanza kukitumia", Mkuu wa mkoa.

Vilevile, mlezi huyo amewataka baadhi ya viongozi wenye tabia ya kuwanyanyasa madereva kama vile kuwatumia muda mwingi pasipo sababu, kuingilia posho za mafuta waache tabia hiyo kwani haina tija zaidi ya kujenga chuki.


Aidha, katika mkutano huo Mkuu huyo wa Mkoa amekipongeza chama hicho kwa kuzidi kujiimarisha kwa kuwa na wanachama wengi kutoka idadi ya 80 hadi 183 na kawataka wale ambao bado hawajajiunga kutoka Ofisini kwake wafanye hivyo haraka.

"Nimesikia katika risala yenu baadhi ya changamoto zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa Ofisi na kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi yenu,natoa maelekezo kwa Katibu Tawala kukaa na uongozi wenu ili kupatikane ufumbuzi na kikao kijacho nipate mrejesho",Mtanda.

Awali katika taarifa yake fupi kwa mgeni rasmi,Katibu wa chama hicho Mkoa,Juma Mago amebainisha bado wanachangamoto kwa baadhi ya waajiri kuwa wagumu kutoa ruhusa kuhudhuria mikutano yao pia amempongeza mlezi wao kwa kuwajali kwa vitendo hali iliyowafanya kuhudhuria kwa wingi katika mkutano wao wa Taifa uliofanyika mwaka jana Jijini Arusha.

Katika kongamano hilo RC Mtanda amekabidhiwa tuzo kutokana na mchango wake bora kwa maafisa usafirishaji wa Serikali mkoani Mwanza,na pia baadhi ya Taasisi za Serikali zimekabidhiwa vyeti kutokana na ushirikiano mzuri wanaotoa kwa chama hicho na wanachama wake

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti