• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAHIDI USIMAMIZI MZURI WA KODI, ELIMU NA KUTAKA MALEZI BORA KWA VIJANA

Posted on: April 11th, 2024

RC MTANDA AAHIDI USIMAMIZI MZURI WA KODI, ELIMU NA KUTAKA MALEZI BORA KWA VIJANA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Aprili 11, 2024 ameshiriki Baraza la Eid El Fetr kama mgeni rasmi na kuahidi usimamizi mzuri wa Kodi bila kuonewa mtu, asisitiza elimu na amewataka wazazi kukumbuka wajibu wao wa malezi bora vijana.

Akizungumza na washiriki wa Baraza hilo kwenye ukumbi wa BoT, Mkuu huyo wa Mkoa amesema hakuna Taifa lolote lililoendelea bila ya kuwa na mpango mzuri wa ulipaji wa kodi hivyo atasimamia kikamilifu na kutanguliza uungwana kwa wafanyabiashara.

"Sipo tayari kuona nguvu ikitumika katika utekelezaji wa sheria za nchi iwe kwa mwananchi yoyote wakiwemo wafanyabiashara, napenda mashauriano zaidi na kuchukua maamuzi," amesema Mtanda.

Kuhusu suala la elimu amesema ni wajibu wa kila mzazi kutimiza haki za watoto wao kwa kuhakikisha wanakwenda shule kikamilifu.

Akizungumza suala la malezi Mtanda amekemea tabia iliyoibuka hivi sasa kwa baadhi ya Wanawake wenye vipato kujigamba wao ni 'SINGLE MOTHER' na kusisitiza malezi bora ni kwa wazazi wote wawili

"Familia yenye malezi bora kwa watoto wao mnaturahisishia hata sisi viongozi kuwaongoza watu wenye weledi wa tabia hivyo Taifa linakuwa na watu waliostaarabika.

Aidha amewakumbusha viongozi wote wa dini kuendelea kuwaombea viongozi wetu wa juu  kuwa na afya njema na hekima ya kuliongoza Taifa letu.

"Rais Samia katuletea miradi mingi ya kimkakati yenye thamani ya ma trioni ya fedha ikiwemo reli ya kisasa SGR,Meli ya Mv Mwanza,Daraja la JP Magufuli na sasa unapanuliwa uwanja wa ndege uwe wa knimataifa,ni wajibu wa kila mmoja kumshukuru na kumuombea",RC Mtanda.

Akimkaribisha mgeni rasmi kwenye Baraza la Eid,Shehe mkuu wa mkoa wa Mwanza,Hassan Kabeke amesema wao kama viongozi wa dini wataendelea kuiunga mkono Serikali katika ujenzi wa Taifa na tayari wana kauli mbiu kwa waumini wao isemayo Shiriki uchaguzi mdogo wa Serikali za mitaa kwa utulivu na amani.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti