• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ACHANGIA MIL.5 MATIBABU YA WATOTO WENYE SARATANI

Posted on: September 17th, 2024

RC MTANDA ACHANGIA MIL.5 MATIBABU YA WATOTO WENYE SARATANI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo septemba 17, 2024 amechangia kiasi cha shilingi milioni tano katika kampeni ya kuwachangia watoto wanaosumbuliwa na maradhi ya saratani (Bugando Health Marathon 2024).

Sambamba na mchango huo, Mhe. Mtanda pia ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa maendeleo Mkoani humo kuungana na Hospitali ya Kanda ya Bugando katika kampeni ya kuwachangia watoto hao ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu wa fedha za matibabu.

Mkuu wa Mkoa huyo ametoa mchango na rai hio alipokutana na Wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Mwanza watakaoshiriki Bugando Health Marathon 2024 itakayofanyika tarehe 20 Oktoba, 2024 iliyolenga kuchangia fedha za matibabu kwa watoto wanaokabiliwa na maradhi ya saratani.

Aidha RC Mtanda amesema Hospitali ya Bugando wao wameamua kuisaidia Serikali kwa kuwa serikali haiwezi kufanya kila kitu hivyo ushiriki wa kampeni hiyo itasaidia kupunguza mzigo kwa serikali.

"Utafiti unaonesha kwamba Mkoa wa Mwanza umekuwa na changamoto ya Watoto wengi wanaokabiliwa na maradhi ya saratani na saratani hizi zikitibiwa mapema basi inaweza kutibika lakini matibabu yake ni gharama sana hivyo ndio maana nimewaiteni ili mtusaidie kutuunga mkono tuweze kuwasaidia watoto wetu". Amesema RC Mtanda.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kanda Bugando Dkt. Fabian Massaga amesema wamedhamiria kukusanya takribani kiasi cha Shilingi Bilioni moja ambapo inakadiriwa kusaidia watoto takribani mia tano wanaokabiliwa na maradhi hayo.

Kadhalika Dkt. Massaga amewaomba wadau hao kujitoa kwa kuwaunga mkono na kubainisha kuwa sadaka watakayoitoa ni thawabu kwao na kwa hao watoto ambao nai wana ndoto za kuishi na kuwataka pia kushiriki katika mbio hizo zinazotarajiwa kuongozwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti