RC MTANDA AFANYA KIKAO NA WAFANYABIASHARA WA VIWANDA VYA SAMAKI
RC MTANDA AFANYA KIKAO NA WAFANYABIASHARA WA VIWANDA VYA SAMAKI
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda mapema leo Februari 19, 2025, ameongoza kikao cha wafanyabiashara wa Viwanda vya Samaki katika Wilaya za Nyamagana na Ilemela na kuagiza sheria ya mabondo ambayo imekuwa ikileta mkanganyiko kupitiwa upya na kusiwepo na ushuru mara mbili kwa wale wachakataji wa mabondo viwandani.




