• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA AWALI JESHI LA AKIBA 2024 SENGEREMA

Posted on: November 17th, 2024

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA AWALI JESHI LA AKIBA 2024 SENGEREMA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo 17 Novemba, 2024 amefunga rasmi mafunzo ya awali ya askari wa jeshi la akiba Kimkoa 2024 yaliyofanyika katika shule ya Msingi Ngoma kata ya Igalula Wilayani Sengerema.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa gwaride lililofana  pamoja na maonesho mbalimbali Mhe. Mtanda amewapongeza wahitimu hao 111 waliohitimu kwa kulinda nidhamu, utii na subira wawapo kwenye mafunzo na hatimaye kuwa rasmi askari wa jeshi hilo kama kiapo chao kinavyowataka.

Aidha, amewataka kudumu kwenye kiapo cha kutetea uchumi wa nchi kwa kushiriki katika vitendo vya kupambana na maadui ujinga, maradhi na umasikini katika jamii wanayoishi kwa kuchapa kazi na kutoa hamasa kwa wananchi kuwa wazalendo na kujibidiisha katika masomo ili kujipatia maendeleo.

Vilevile, ametoa wito kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuhakikisha wanawapatia vijana hao mikopo ili wafanye shughuli za ujasiriamali na wawajengee uwezo hatimaye kuunda makundi yatakayokidhi sifa za utoaji wa mikopo kupitia makundi ya vijana, wanawake na wenye ulemavu.

"Katika uchaguzi wa Serikali za mitaa viongozi na wagombea wote nawasihi mkajiepushe na rushwa kwani ni adui wa haki na kiongozi anayepatikana kwa kutoa rushwa hatowahudumia wananchi kwa moyo wote bali atakua ni mtafuta maslahi." Amesema Mhe. Mtanda alopokuwa akizungumzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Naye Mshauri wa jeshi la akiba Sengerema Meja Erick Mateni mesema kuwa vijana hao wataimarisha ulinzi katika maeneo yao kutokana na ukakamavu na uzalendo waliopewa kama vile mbinu za kivita, usomaji wa ramani, ujasiriamali, uraia, usalama wa habari, madhara ya rushwa pamoja na kuzima moto.

Wakisoma risala wahitimu hao Lily Simon na Magreth Edward wametoa ombi la kupewa kipaumbele kwenye kazi za ulinzi hususani kwenye mgodi wa Sota Mining pamoja na kupatiwa mikopo kupitia kundi la vijana, wazee na wenye ulemavu katika Halmashauri.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti