• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA

Posted on: March 28th, 2025

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Machi 28, 2025 amefunga mafunzo ya ufugaji wa samaki kwa njia ya Vizimba na kutoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo ya siku 15 kwenye chuo cha wakala wa Elimu ya Uvuvi Feta, Nyagezi wilayani Nyamagana, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa hakuna sababu za vijana kukaa vijiweni wakati zipo fursa mbalimbali za kuwainua kiuchumi.

Amesema Serikali ya awamu ya sita kwa kutambua nguvu kazi ya vijana imetoa fedha nyingi katika mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ambao umekuwa na tija katika awamu hii ya kwanza.

"Jumla ya boti 160 za kisasa za uvuvi zimetolewa kwa wanufaika 3, 295 na vizimba 222 kwa wanufaika 1,214 na mikopo hiyo imetolewa bila riba na benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania TADB", Mhe. Mtanda

Aidha amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuja na mageuzi chanya baada ya kupata mafunzo hayo hasa kuongeza Uzalishaji wa samaki ambao takwimu zinaonesha bado upo chini kutokana na sababu mbalimbali ukiwemo uvuvi haramu na tabia nchi.

Mhe.Mtanda ameipongeza pia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuandaa mafunzo hayo yenye lengo la ukuzaji viumbe maji na pia kukuza biashara kupitia rasilimali hizo.

Ameongeza kuwa bado ulaji wa samaki kwa  mtanzania kwa mwaka upo chini ambao ni kilo 7-8 wakati inatakiwa ulaji uwe kilo 20,hivyo mafunzo hayo yatakuwa ni muarobaini wa changamoto hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa Kampasi ya Mwanza kutoka chuo cha wakala wa Elimu ya Uvuvi FETA Bw.Steven Lukanga amesema kwa siku 15 washiriki hao wamejifunza ukuzaji wa samaki kibiashara na masoko yake,kuhakiki ubora wa maji,afya na magonjwa ya samaki,mfumo wa ukuzaji wa samaki na utengenezaji wa vyakula na Uzalishaji samaki kwenye vizimba.

"Tunaishukuru Serikali kwa kuendelea kuiinua na kuiboresha sekta ya Uvuvi hapa nchini,ombi letu kama chuo itambuliwe mipaka kati ya wavuvi wa asili na wenye vizimba kutokana na kuibuka kwa migogoro ya mara kwa mara",Makanga.

Jumla ya washiriki 172 ambao ni wafugaji samaki na Maafisa Uvuvi kutoka mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na Dar-e-s-Salaam,Lindi,Morogoro na Pwani wamepata mafunzo hayo na kutunukiwa vyeti.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti