• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AHIMIZA KULIOMBEA TAIFA, KUTENDA MEMA NA KUWAKUMBUKA WASIO NA UWEZO

Posted on: April 10th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA KULIOMBEA TAIFA, KUTENDA MEMA NA KUWAKUMBUKA WASIO NA UWEZO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Aprili 10, 2024 ameungana na waumini wa dini ya kiislamu katika swala ya Eid iliyofanyika kwenye uwanja wa Nyamagana na kuwakumbusha kuendelea kuliombea Taifa kujenga mshikamano, kutenda matendo mema na kuwakumbuka wale wasio na uwezo na hatimaye kupata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Taifa la Tanzania limeendelea kuwa na amani kutokana na busara na hekima za viongozi wetu wa juu hivyo hakuna budi kuwaombea ili Mwenyezi Mungu awazidishie ari ya kuwatumikia vizuri Watanzania.

"Wapo baadhi ya watu wanapokuwa kwenye nafasi huzitumia vibaya iwe kwa dhuluma au uonevu wa aina yoyote mambo ambayo hayampendezi Mwenyezi Mungu aliyetuleta Duniani ili tumtumikie vyema na kurejea kwake tukiwa wasafi wa roho," Mkuu wa mkoa.

Mara baada ya kushiriki swala ya Eid Mhe. Mtanda akiongozana na Shekhe Mkuu wa mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke pamoja na wadau benki ya NMB wakiwa kwenye Ofisi za Bakwata mkoa, wametoa zawadi ya sikukuu kwa vituo 11 vya watoto wanaoishi katika mazingira magumu kutoka wilaya Nyamagana na Ilemela zenye thamani ya shs milioni 2.6

"Mhe.mkuu wa mkoa tunakushukuru sana kwa tendo hili,hizi fedha ulizogharamia pengine ungeamua kula vizuri na familia yako,lakini ukaamua kuzitoa kwa ajili ya wengine,Mwenyezi Mungu azidi kukupa rehema zake," Shehe Kabeke.

Akimshukuru mkuu wa mkoa kwa zawadi hizo, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi amesema watoto hao wanaendelea kujiona ni wa famllia moja kutokana na Jamii kuwa nayo karibu kwa kuwapa misaada mbalimbali.

Akiwa katika Iftar iliyoandaliwa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala Jumanne hii jioni kwenye Hotel ya City Link,mkuu huyo wa mkoa amesema Ofisi yake ipo wazi wakati wote kuwasikiliza  wale wenye kero mbalimbali.

"Mimi siyo mkaaji wa ofisini bali nitawafuata huko mlipo wananchi na wale mtakaofika ofisini kwangu mjisikie huru kuniona lakini sitaki kuletewa taarifa chonganishi," amesisitiza Mhe.Mtanda wakati akitoa hotuba fupi mara baada ya Iftar.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti