• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MFUMO WA GoTHOMIS NA LISHE

Posted on: March 12th, 2025

RC MTANDA AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MFUMO WA GoTHOMIS NA LISHE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amefungua kikao cha kamati ya afya ya msingi mkoani humo na kuhimiza utekelezaji wa mfumo wa taarifa za usimamizi wa uendeshaji wa afya wa Serikali ya Tanzania katika vituo vya huduma za afya(GoTHOMIS) na afua za Lishe lengo likiwa Mkoa huo uwe kinara Kitaifa katika utoaji bora wa huduma hizo.

Akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo leo Machi 12, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, Mtanda ametoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha mfumo huo unafungwa kwenye vituo vyote vya afya na apatiwe taarifa ya maendeleo yake kabla na baada ya matumizi hayo.

Amesema kwa mujibu wa takwimu Mkoa wa Mwanza unashika nafasi ya 3 kitaifa kwa utekelezaji wa huduma ya GoTHOMIS, amehimiza kazi ya ziada iendelee kufanyika ili tushike nafasi ya kwanza.

"Serikali inaendelea kuwekeza katika miradi ya afya, lakini hatuna budi kuhakikisha yanakuwepo makusanyo sahihi ya fedha ili zisaidie kuboresha huduma hiyo na nyinginezo", Mkuu wa Mkoa.

Kuhusu afua za Lishe, Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha maafisa lishe kutoka halmashauri zote mkoani humo kuhakikisha wanafanya vizuri ili kuepukana na hali ya udumavu na ukosefu wa afya kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

"Hapa Afisa Lishe Mkoa ametupitisha katika taarifa yake bado Halmashauri nyingi hazifanyi vizuri,na hili ni agizo la Mhe.Rais kwa sisi wakuu wa mikoa kulisimamia vizuri zoezi hili,sasa sitakuwa tayari kuona baadhi ya maafisa lishe mkifanya uzembe,"amesisitiza Mtanda wakati akifunga kikao hicho.

Wakati huo huo, Waziri wa Afya Mhe. Jenister Mhagama amepata wasaa wa kuwasalimu wajumbe wa kikao hicho alipofika Ofisi ya mkuu wa mkoa akielekea katika majukumu mengine na kusisitiza bado magonjwa yasiyoambukiza ni changamoto na kutoa rai kubadili mtindo wa maisha ukiwemo ulaji na kufanya mazoezi.

Kikao cha kamati ya afya ya msingi ya Mkoa kimewajumuisha wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa Halmashauri, waganga wakuu wa wilaya,maafisa lishe pamoja na viongozi wa dini.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti