• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AHIMIZA WELEDI KWA WAKANDARASI WAZAWA MIRADI YA SERIKALI,AZITAKA TAASISI KUJENGA VIWANJA VYA MICHEZO

Posted on: August 5th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA WELEDI KWA WAKANDARASI WAZAWA MIRADI YA SERIKALI,AZITAKA TAASISI KUJENGA VIWANJA VYA MICHEZO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Agosti 5,2024 amefanya ziara fupi ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar-e-s Salaam Tawi la Mwanza unao gharimu shs bilioni 37 unatekelezwa na Mkandarasi mzawa Kampuni ya Comfix Engineering na kuhimiza weledi katika miradi ya Serikali.

Mkuu huyo wa Mkoa akiwa na mkurugenzi wa tawi hilo Dkt.Albert Mmari amejionea hatua ya umaliziaji wa majengo manne ya ufundishaji,Taaluma na hosteli za wanaume na wanawake pamoja na uwanja wa michezo wa siku nyingi wa tawi hilo na kutaka uboreshwe ili uje kuwa na tija zaidi.

"Nimefurahishwa na uwanja huu na hapa naomba nitoe msisitizo,Taasisi zote za Serikali na binafsi jengeni viwanja vya michezo nchi yetu ipo mbioni kuwa mwenyeji wa michuano ya AFCON 2027 na huenda CCM Kirumba ukatumika mtajiongezea vipato timu zikija kufanya mazoezi,"amesisitiza Mtanda.

Amesema katika michuano ya ligi kuu ya NBC timu mbalimbali zitafika kucheza na Pamba Jiji FC na wakati zinajiandaa na mechi zitahitaji viwanja vya mazoezi.

Akizungumza kampuni za watanzania kupewa miradi mikubwa ya Serikali,Mtanda amesema ni wajibu wao kutanguliza uaminifu na kuikamilisha kwa wakati hali ambayo itawajengea kuaminiwa na Serikali.

"Huu mradi wa miundombinu hii uliogharimu fedha nyingi ni mfano mzuri kwa mkandarasi huyu,kila jengo naambiwa linakamilika mwaka huu,endeleeni na weledi huu,"Mtanda

Kwa upande wake mkurugenzi wa tawi hilo Dkt.Albert Mmari amesema ujenzi huo una malengo makuu matatu kuongeza udahili,kuongeza programu ya elimu ya ufundi na ushirikiano wa kikanda.

"Mara baada ya mradi huu kukamilika utakuwa na tija kwa nchi za Afrika Mashariki na kati kwa watu kuja kupata utaalamu wa juu namna ya kuzalisha bidhaa za ngozi,"Dkt.Mmari

Ujenzi huo wa majengo ya kisasa ulioanza mwaka 2019 na utakamilika mwaka huu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti