• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AMPOKEA NAIBU WAZIRI WA MAJI MWANZA

Posted on: July 24th, 2024

RC MTANDA AMPOKEA NAIBU WAZIRI WA MAJI MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Julai 24, 2024 Ofisini kwake amempokea na  kufanya mazungumzo mafupi na Naibu Waziri wa Wizara ya Maji Mhandisi Kundo Mathew aliyefika mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametumia wasaa huo kuipongeza Wizara hiyo kwa juhudi za kupunguza adha ya maji kwa wananchi kwa kutekeleza miradi kadhaa huku akitolea mfano wa kazi nzuri inayofanywa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA).

"Tuna chanzo kipya cha Butimba na kwasasa changamoto yetu ni kwenye usambazaji, naamini mkandarasi yupo kazini kwa ajili ya upanuzi wa usambazaji kutoka kwenye chanzo cha Butimba kupitia fedha zaidi ya Bilioni 49 zilizotolewa na Shirika la maendeleo la ufaransa." Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Mtanda ametoa wito  MWAUWASA kuhakikisha wanasimamia ulipwaji wa fedha zilizobaki kwenye chanzo cha mradi wa maji wa Butimba na ikiwezekana waongeze pampu ili kuongeza uzalishaji wa maji.

Vilevile, amewasihi kuendelea kusimamia miradi ya usafi wa mazingira na maji taka ili kuwahakikishia afya njema wananchi wa Mkoa wa Mwanza ambao wana matumaini makubwa na huduma bora za kijamii zinazotekelezwa na Serikali ya awamu ya sita.

"Kazi yoyote ni ibada na ibada njema ni kufanya kitu kwa utimilifu wake hivyo naamini watumishi wa sekta ya maji wataendelea kujituma ili kuhakikisha wanawatumikia wananchi." Mkuu wa Mkoa.

Naye, Naibu waziri Mathew amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa Wizara hiyo itaendelea kupokea na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi na kwamba watahakikisha usambazaji maji vijijini unafikiwa kwa asilimia 85 ili kuinua uchumi wa wananchi.

"Sekta ya maji imebadilika sana nasi kama Wizara tunaendelea kufanya ufuatiliaji wa kina kutokana na msukumo wa Mhe. Rais ambaye amedhamiria kumtua mama ndoo kichwani iliyopelekea kupatikana kwa sheria namba tano ya 2019 ambayo imewazaa RUWASA" Mhe. Waziri.

Aidha, amewataka Mamlaka za maji mkoani humo kutengeneza mfumo mzuri wa kupata taarifa zinazohusu changamoto za maji kutoka ngazi za vitongoji hadi juu ili wawafikie na kurekebisha kwa haraka.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti