• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ASHUHUDIA SAFARI YA KWANZA YA MV NEW MWANZA KWENDA BUKOBA

Posted on: September 21st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 21 Septemba, 2025 ameshuhudia jaribio la mwisho la safari ndefu kwa Meli ya MV New Mwanza kwenye bandari ya Mwanza Kusini iliyopo jijini Mwanza ilipoondoka kuelekea kwenye Bandari ya Bukoba (Neutical Miles 100).

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kushuhudia hafla hiyo ya kihistoria Mhe. Mtanda amesema kukamilika kwa meli hiyo ni ishara ya juhudi za serikali katika kuimarisha sekta ya usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo katika ukanda wa ziwa Victoria.

Aidha, amesema wananchi wa Mwanza na ukanda wa ziwa Victoria kwa ujumla wamepata usafiri wa uhakika kwani Mhe. Rais Samia amedhamiria kuwaondoka kwenye adha ya ajali zilizotokana na matumizi ya usafiri duni wa mitumbwi na kwamba nauli zitakua nafuu sana kwa safari za ndani na nje ya nchi.

Ameongeza kuwa katika kuhakikisha katika ukanda huo kunakua na usalama katika usafiri, usafirishaji na hata uvuvi serikali kwa kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya Afrika Mashariki wanajenga kituo maalum cha uokozi katika eneo la Malaika Beach kwa gharama ya zaidi ya Bilioni 5.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Meli nchini (TASHICO) Bw. Eric Hamissi amebainisha kuwa Ujenzi wa meli hiyo umefikia asilimia 99 na baada ya safari hiyo ya Mwanza- Kemondo hadi Bukoba wanatarajia kupata majibu ya ufanisi wake kitaalamu na mara moja kuanza safari katika Ziwa Victoria.

Amesema, pamoja na changamoto kama za kupanda kwa gharama za vifaa kama vya vyuma na wataalamu kushindwa kufika kwa wakati hatimaye meli hiyo ya kisasa yenye urefu wa mita 92.6 yenye spidi kubwa leo hii imekamilika na itafika Bandari ya Bukoba kwa saa 6 pekee.

Aidha, amebainisha kuwa meli hiyo yenye uzito wa tani elfu nne (4000) na ghorofa nne, ina uwezo wa kubeba abiria 1200, Magari 20 madogo, Malori 3 imejengwa na watanzania zaidi ya 200 walioshirikiana na timu ya wataalamu 16 tu  wa mkandarasi kutokea nchini Korea Kusini.

"Kwa mara ya kwanza Meli hii itafika katika bandari ya Bukoba na italala huko na kesho itarejea Mwanza na imejengwa kwa zaidi ya Tshs. Bilioni 120 ambapo ni lazima tumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ameikuta kwenye 40% tu ya ujenzi mwaka 2021 huku zikiwa zimelipwa Tshs. Bilioni 36 pekee lakini amemalizia fedha zote." Amebainisha Mkurugenzi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti