• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ATAKA GHARAMA ZA MAJI KUWA RAFIKI KWA WANANCHI

Posted on: September 18th, 2024

RC MTANDA ATAKA GHARAMA ZA MAJI KUWA RAFIKI KWA WANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewaagiza Wakala wa Maji vijijini (RUWASA) Mkoani humo kushirikisha wananchi kupitia vikao kupata bei za Maji zilizo rafiki kwa hali zote ili lengo la miradi hiyo kusaidia jamii litimie.

Ametoa kauli hiyo leo jumatano tarehe 18 septemba, 2024 akiwa kwenye Kijiji cha Kahangara Wilayani Magu wakati akikagua maendeleo ya mradi wa ukarabati maji uliotekelezwa na serikali kupitia Mradi wa Uviko 19 kwa zaidi ya Tshs. Milioni 508.

Mhe. Mtanda amewataka RUWASA kupitia wasimamizi wa jumuiya za watumia maji kutokupandisha bei za maji kiholela kwani kwa kufanya hivyo ni kwagombanisha wananchi na Serikali yao na kuwataka kuendelea kutoza bei ambazo ziliamuliwa na mikutano ya kijiji tu na si vinginevyo.

Mhe. Mtanda amesema serikali ya awamu ya sita inatekeleza miradi ya huduma za jamii hususani Maji kama unavyotarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kutoka asilimia 34 hadi 90 hivyo watendaji ni lazima wasimamie ukamilifu wa hilo.

Aidha, amewataka RUWASA kuhakikisha kuwa kupitia mradi huo wanafikisha huduma za maji kwenye vijiji vyote ambavyo bado havijapata maji safi na salama ndani ya kata hiyo na kusimamia miundombinu hiyo ili maji yaendelee kutoka kila siku.

Meneja RUWASA Wilaya ya Magu Mhandisi Daud Amlima amebainisha kuwa mradi huo umeshakamilisha vituo 34 vya kuchotea maji ambayo vinatoa maji na kwamba unasimamiwa na wananchi wenyewe kupitia jumuia zao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti