• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ATOA SOMO KWA WATENDAJI KUCHUKUA HATUA KUREKEBISHA MATATIZO BUCHOSA

Posted on: January 20th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefika katika Kituo cha Afya Nyamsenda kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa na kutoa somo la uwajibikaji kwa Viongozi na Wataalamu baada ya kubaini kuwa wamekua wazembe katika kuchukua maamuzi.

Akikagua ujenzi wa majengo ya Mama na Mtoto, upasuaji, nk Mkuu wa Mkoa amejikuta akiingia kwenye fatiki ya kuondosha mifuko ya saruji katika makazi ya mtumishi anayeishi kwenye chumba kimoja kutokana na chumba kingine kujazwa saruji zilizoganda ambazo hazifai tena kwa matumizi.

Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa mnamo juni 03, 2021 serikali ilileta Tshs. Milioni 250 katika kituo hicho cha Afya kwa ajili ya ujenzi lakini pamoja na kukamilika kwa ujenzi kulitokea uzembe uliosababisha mifuko kadhaa ya saruji kaganda na kwamba waliosababisha walishachukuliwa hatua za kinidhamu.

Aidha, Halmashauri hiyo iliendelea kubaki na mifuko hiyo na kuamua kuihifadhi kwenye nyumba ya mtumishi na kusababisha adha ya kuharibu faragha kwenye kaya hiyo yenye watoto wawili ambao walilazimika kulala na wazazi wao.

Halikadhalika Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kufanya tathmini na kukarabati nyumba hiyo ndani ya siku saba ili kumpatia mazingira safi na salama ya kuishi mtumishi huyo pamoja na familia yake.

Juma Lugendo, Msaidizi wa Afya katika kituo hicho ambaye ni mtumishi anayeishi kwenye chumba kimoja katika nyumba yenye vyumba 2 kutokana na kimoja kugeuzwa kuwa stoo ya kuhifadhia saruji iliyoganda amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa maamuzi ya kuondoa saruji hiyo.

Aidha, ameonesha furaha yake na kubainisha kuwa kwa sasa ataishi na familia yake kwa furaha kwani hawatakua na woga wa kuingiliwa na wadudu lakini pia kwa kuondokana na athari za kiafya ambazo wangeweza kuzipata yeye na familia yake.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti