• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ATOA SOMO UMUHIMU WA SADAKA

Posted on: March 30th, 2025

RC MTANDA ATOA SOMO UMUHIMU WA SADAKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameikumbusha jamii umuhimu wa kutoa sadaka kwa moyo mkunjufu kwani kwa kufanya hivyo ndio maombi na sala zinaweza kupokelewa na kujibiwa kwa haraka zaidi na Mwenyezi Mungu.

Ameyasema hayo leo machi 30, 2025 alipokuwa akizungumza katika  Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Katoliki la Parokia ya Bikira Maria Msaada wa Daima- Kome, Wilaya ya Sengerema Jimbo la Geita. Harambee iloyofanyika katika ukumbi wa Gold Crest Hotel, Jijini Mwanza.

"Katika changizo hili naomba tutoe kwa imani tukiamini kwamba Mungu atatusaidia kwa mambo mbalimbali kama magonjwa, migogoro ya ndoa hivyo toa kwa imani kuwa natoa sadaka hii ila Mungu maliza mgogoro wangu wa ndoa, Hivyo toa huku ukiomba”. Mhe. Mtanda

Aidha Mkuu wa Mkoa ameendelea kwa kusema unapotoa sadaka yakupasa kutoa kwa imani na sio kwa manung'uniko, amesema usitoe kwa sifa wala manung'uniko ni mambo ambayo Mungu ameyakataza.

“Na kama umegombana na ndugu yako kabla ya kutoa sadaka yako kapatane nae kwanza ili ubarikiwe. Ukitoa unapata heri na unaweka hazina yako mbinguni." - Mkuu wa Mkoa.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa pia ameitaka jamii kutoa sadaka kutokana na uwezo yaani isizidi wala isipungue kiwango ambacho mtu anakipata aidha amesema na ndio maana kuna sadaka inaitwa zaka ambayo huitajika 10% tu ya mapato na haitakiwi kupungua wala kuongezeka.

Naye Mhashamu Baba Askofu Flaviana Kassala Askofu wa Jimbo Katoliki Geita amesema harambee hiyo ya ujenzi wa kanisa Katoliki inatokana na umuhimu wa kanisa hilo na historia iliyopo ambapo mpaka sasa kanisa hilo limefikisha miaka 125, hivyo ujenzi huo unahusisha kulinda historia ya Kanisa na kisiwa cha kome.

“Ujenzi wa kanisa hili si kwa ajili ya Kanisa tu bali imebeba historia yetu kama Taifa, ambapo hapo awali miaka ya 1900 ilisaidia kuimarisha mahusiano kati yetu na wageni waliotoka nchi za ulaya kuleta injili”.

Aidha Mhashamu Baba Askofu ameendelea kwa kusema kisiwa cha kome kina vivutio na matarajio mengi hivyo kusherehekea miaka hiyo 125 ni kulinda  pia tunu na historia ambayo kisiwa hicho kinabeba.

Awali Harambee hiyo ilikusudia kupatikana kwa shilingi milioni 500, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amechangia kiasi cha shilingi milioni 5, huku jumla kuu ya fedha taslimu na ahadi ni shilingi milioni 177. Aidha sherehe ya miaka 125 ya Kanisa hilo inatarajiwa kufanyika Agosti 17 mwaka huu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti