• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ATOA WITO KWA WANAWAKE KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

Posted on: March 6th, 2025

RC MTANDA ATOA WITO KWA WANAWAKE KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi nchini katika uchaguzi mkuu 2025 kwani Serikali imejipambanua kwenye kukuza usawa, haki na uwezeshaji kwa jamii.

Mhe.Mtanda ametoa wito huo mapema leo Machi 06, 2025 kwenye uwanja wa mpira wa Nyamagana wakati akihutubia wanawake na wananchi walioshiriki maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya wanawake ngazi ya Mkoa.

Mtanda amesema wanakwake ni jeshi kubwa nchini hivyo likitumika vizuri litaleta maendeleo na Serikali inaendelea kutoa usawa wa kijinsia kwenye uongozi na ndiyo maana hata Mwanza wapo viongozi wengi wa kike na 43% ya viongozi ni wanawake nchini.

"Tunazo bilioni 2.4 kwa ajili ya mikopo kwa walemavu tena kwa jinsia zote na kundi hili siyo lazima waombe mkopo kwa vikundi hata mmoja mmoja na jumla ya wataalamu wa afya 3201 wameajiriwa kuanzia 2021 hadi 2025 na kufanya huduma za afya kuimarika zaidi mkoani Mwanza." Mhe. Mtanda.

Akisoma risala ya wanawake wa Mkoa huo Mwalimu Sophia Turuya amesema wanawake nchini ni wengi zaidi ya wanaume kwa uwiano wa zaidi ya milioni moja hivyo kundi hilo likipewa fursa litakua ni chachu ya maendeleo.

Aidha, ameipongeza Serikali kwenye uboreshaji wa huduma za afya na akawasilisha ombi la kuongezwa kwa wataalamu wa afya na mazingira pamoja na kuweka mazingira rafiki ya kupata nishati safi ya kupikia pamoja na mabweni ya wasichana ili watoto wa kike wasome katika mazingira salama.

Vilevile, ameutaja mfuko wa maendeleo ya wanawake kupitia vikundi vya ujasiriamali kama mkombozi wa mikopo kwa masharti nafuu kwa wanawake ambao unawapatia mitaji kupitia mikopo itokanayo na mapato ya ndani ya halmashauri.

Katika kunogesha maadhimisho hayo yenye kauli mbiu 'wanawake na wasichana 2025, tuimarishe haki, usawa na uwezeshaji' michezo mbalimbali imerindima kama kuvuta kamba, mbio kwenye magunia, kufukuza kuku na washindi wamejipatia zawadi nono.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti