• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AUTAKA UONGOZI WA ATCL KULETA NDEGE ZAIDI MWANZA KUBORESHA USAFIRI

Posted on: July 3rd, 2024

RC MTANDA AUTAKA UONGOZI WA ATCL KULETA NDEGE ZAIDI MWANZA KUBORESHA USAFIRI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda ameutaka uongozi wa Shirika la ndege nchini ATCL kuongeza idadi ya ndege  mkoani humo kutokana na idadi ya abiria kuzidi kuongezeka hali inayosababisha kuwepo na ugumu wa kupata usafiri huo kirahisi.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa rai hiyo leo Julai 03, 2024 wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa chumba maalum cha abiria wa daraja la juu la biashara iliyofanyika eneo la uwanja wa ndege, Mtanda amebainisha kutokana na Jiji la Mwanza kuwa eneo la kimkakati ongezeko la usafiri wa anga limezidi kuongezeka.

"Mkurugenzi Mhandisi Matindi nalisema hili mbele yako, sasa hivi ukitaka kuondoka leo hii kutoka Mwanza kwenda Dar siyo rahisi kupata usafiri ni lazima ufanye utaratibu siku mbili kabla, sasa hii katika soko la ushindani itawaletea shida," amesema Mtanda.

Mkuu huyo wa Mkoa amezitaka Shirika hilo kuzidi kujiimarisha na kuepuka usitishaji wa safari kiholela ili kuzidi kujiaminisha kwa huduma bora kwa wateja wake, kwani mashirika makubwa ya kimataifa ndege yatakapoanza safari zake kuanzia uwanjani hapo waweze kuumudu ushindani.

"Nampongeza Rais Samia kwa kuendeleza mazuri kwenye Shirika hilo yaliyofanywa na watangulizi wake, ametoa shs bilioni 13 kujenga jengo la kisasa la abiria, hivi sasa mkandarasi Taifa yupo eneo la ujenzi kulikamilisha jengo hilo litakalo chukua abiria wa kigeni 600 kwa mkupuo na wazawa 800," Mhe. Mtanda.

Aidha Mtanda amelishauri ATCL kuona umuhimu wa kuweka safari ya moja kwa moja kutoka Mwanza hadi Makao makuu ya nchi Dodoma, kuliko ilivyo sasa abiria kulazimika kushukia Dar na kwenda Dodoma.

"Haiwezekani kushindwa kuwepo na muunganiko wa safari ya moja kwa moja kwenda makao makuu ya nchi ni lazima muone hadhi ya Dodoma na wapo abiria wengi wanaohitaji usafiri huo," amehimiza Mtanda wakati wa hafla hiyo fupi.

Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi amesema wanatambua mchango mkubwa wa kibiashara wa Mkoa wa Mwanza na wapo katika mkakati wa kuboresha usafiri kutokea mkoani humo

"Hivi sasa tuna ndege 14 na tupo mbioni kupata ndege nyingine moja, tuna imani changamoto zilizopo zitamalizika na huduma zetu zitazidi kuimarika", amesema Mhandisi Matindi.

ATCL iliyoanzishwa mwaka 1977 baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wameingia mkataba wa huduma hiyo ya chumba cha daraja la juu la abiria wa biashara na VIA Aviation kwa miaka 2 na wapo mbioni kuanzisha huduma hiyo uwanja wa ndege wa Dodoma.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti