• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWAKABIDHI VYETI VIJANA WA HALAIKI KILELE CHA MWENGE WA UHURU 2024, AKEMEA UTORO SHULENI

Posted on: March 13th, 2025

RC MTANDA AWAKABIDHI VYETI VIJANA WA HALAIKI KILELE CHA MWENGE WA UHURU 2024, AKEMEA UTORO SHULENI


Leo tarehe 13 Machi, 2024 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewakabidhi vyeti vijana walioshiriki kwenye halaiki wakati wa kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba tarehe 14 Oktoba, 2024.

Akiongea na vijana hao Mhe. Mtanda amewataka kuacha tabia ya utoro shuleni na badala yake wadumishe nidhamu na uzalendo ili kuendelea kuwa bora kitaaluma ili waweze kupata ufaulu mzuri utakaowasaidia kujitegemea katika maisha ya baadaye.

Aidha, amefafanua kuwa ndani ya muda huo mkoani Mwanza yamejengwa madarasa 306 ya shule za msingi, madarasa 2110 kwa Sekondari, matundu ya vyoo kwa msingi 1265 pamoja nyumba za walimu kwa msingi na Sekondari zaidi ya 80 zimejengwa pamoja na walimu 8465 wa msingi na Sekondari kupandishwa madaraja.

"Ndani ya miaka mitano ya uongozi wa Rais Samia mkoani Mwanza umejengea shule mpya 45, wanaodhani maendeleo nchini hakuna hawajatoka nje wakaona jinsi wenzetu wanavyoteseka lakini sisi tunasonga mbele tena kwa kasi." Mhe. Mtanda.

Amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita imejitanabaisha kuendelea kusimamia na kugharamia programu mbalimbali za elimu kuanzia ngazi ya awali hadi kidato cha sita kwani Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ana nia ya dhati ya kumpatia elimu bora kila mtanzania.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwashukuru wazazi na walezi walioruhusu watoto wao kushiriki tukio hilo la kizalendo pamoja na wakufunzi wa kitaifa walioongozwa na ndugu Philipo Chogolela kwa kufanikisha halaiki mujarabu iliyoakisi nidhamu, ukakamavu na uzalendo.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amesema vijana zaidi ya 1350 walishiriki halaiki kwenye kilele cha mbio za mwenge wa uhuru 2024 kwa hamasa kubwa na kwa uzalendo ambapo walifundishwa kwa siku 60 na wakufunzi wa kitaifa na wa ndani.

"Mwanza hatuna jambo dogo, tulivunja rekodi kwa halaiki ya watoto hawa kwani ilifana sana na wageni na wenyeji walifurahia ukamamavu na ubunifu wa kutengeneza maumbo yaliyosawiri miradi ya kimkakati na waliimba wimbo wa kusifu Mkoa na walicheza ngoma ya kabila la wasukuma." Ndugu Elikana.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti