• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWAKARIMU MADIWANI KUTOKA ARUSHA JIJI

Posted on: September 17th, 2024

RC MTANDA AWAKARIMU MADIWANI KUTOKA ARUSHA JIJI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo septemba 17, 2024 amewatembelea Wahe. Madiwani, Wataalamu na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha waliowasili Mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi na kujifunza mambo mbalimbali.

Mhe. Mtanda amekutana na Wahe. Madiwani hao katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuwakaribisha Mwanza kisha kuwataka kutembelea maeneo mbalimbali ya kiutalii ili watakaporudi Mkoani Arusha wakayaelezee yale yote mazuri waliyokutana nayo Mkoani Mwanza.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Mwanza ni Mkoa mkubwa namba mbili kwa idadi ya watu pamoja na muingiliano wa shughuli nyingi za kiuchumi hivyo kuchagua Mkoa wa Mwanza hawajakose kwani ni eneo sahihi la kujifunzia, na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Waheshimiwa hao ambao pia wengi wao anafahamiana nao kwa kuwa aliwahi kufanya nao kazi wakati alipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha mwaka 2021 - 2023.

Sambamba na hayo amewataka Wahe. hao kama watapata nafasi wasisite kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Mkoa wa Mwanza ambayo serikali imetoa fedha nyingi kuhakikisha miradi hiyo inatekelezeka ili kurahisisha huduma kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza, Mikoa jirani pamoja na Nchi jirani.

Naye Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha Mhe. Maximilin Iranqe amemshukuru Mhe. Mtanda kwa ukarimu wake na kutenga muda kuwatembelea Waheshimiwa hao licha ya kuwa na ratiba ngumu, Aidha amemuhakikishia kuwa wataenenda kama alivyowashauri na kumalizia kwa kumtaka kuendelea kushirikiana nao kwa kipindi chote watakapowepo Jijini humo.

Wahe. Madiwani pamoja na Wataalamu hao wamefika Mwanza kwa lengo la kujifunza; Usimamizi na uendeshaji wa stendi ya Nyamhongolo, Uendeshaji wa vikao kwa mfumo wa e-board, Uendeshaji wa jengo la kibiashara la Rock City Mall, Usimamizi na ukusanyaji wa leseni za biashara, kodi ya pango na ushuru wa nyumba za kulala wageni.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti