• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWAKUMBUSHA WANANCHI KUWAJALI WATOTO YATIMA

Posted on: March 26th, 2025

RC MTANDA AWAKUMBUSHA WANANCHI KUWAJALI  WATOTO Yatimie


Leo Machi 26, 2025 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said GB Mtanda ameandaa Iftar kwa Watoto Yatima wanaolelewa kwenye vituo vya Watoto Yatima katika Mkoa wa Mwanza ikiwa ni sehemu ya Ibada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Mkuu wa Mkoa amesema lengo la kufanya iftar hiyo ni kutii maagizo ya Mwenyezi Mungu ambaye yeye mwenyewe amesema mtu yeyote anaewakimbilia yatima na wajane basi amefunga hesabu na Mwenyezi Mungu.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema imekuwa mazoea kwa kutoa iftar na chakula lakini yeye amekuja na wazo la kuboresha maisha na makazi ya watoto kwa kuwa wamekuwa wakiishia kupata chakula tu lakini mazingira wanayoishi ni mabovu.

“Tumekubaliana kuwa tutafanya utafiti tuone ni vituo gani vina uhitaji wa maboresho ya makazi au uhaba wa vitu kama vile vitanda, magodoro na vifaa vingine kisha tuone tunawasaidiaje”.

Kadhalika ametumia wasaa huo kuendelea kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuitunza amani na kuendelea kuliombea Taifa, Viongozi na Serikali kiujumla chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili Taifa liendelee kuwa salama.

Naye Shekhe wa Mkoa wa Mwanza Alhajj Hassan Kabeke amemshukuru Mkuu wa Mkoa kuendelea kufanya mambo makubwa na siyo kufturisha tu bali pia kwa kuwaandalia watoto hao mahitaji mbalimbali muhimu ambayo pia itawaondolea mzigo walezi na wahisani wa watoto hao kwa kipindi fulani.

“Lakini pia Mtume wetu S.W.S anasema nyumba yoyote ambayo yatima atatendewa mema viumbe wa mbinguni wataona nyota inang’aa na nina hakika kwa hadithi hii ya Mtume huko juu wanaulizana hiyo nyota ni ya wapi wanajibiwa ni Mwanza na huyo ni Said Mtanda ametambua nafasi ya Yatima”.

Umefanya vyema Mkuu wa Mkoa ninakupongeza sana. Ameongeza Shekhe Kabeke.

Wakizungumza katika nyakati tofauti tofauti Viongozoi wa Taasisi za kifedha Mwanza walioshirikiana na Mkuu wa Mkoa katika kuandaa Iftari hiyo wamemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa iftar hiyo ya Yatima na kuwaleta pamoja kushiriki ibada hiyo muhimu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti