• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WAKANDARASI WA UMEME MWANZA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Posted on: February 2nd, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amepokea rasmi utambulisho wa wakandarasi wapya wa kupeleka umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya Mkoa wa Mwanza chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kipindi cha miaka mitatu.

Wakandarasi hao ni White City International Contractors Ltd na Tibea Company Ltd, ambao wamesaini mikataba miwili ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa unaolenga kusogeza huduma ya umeme kwa wananchi wa vijijini na maeneo ya pembezoni.

Akizungumza wakati wa utambulisho huo, Mhe. Mtanda amewataka wakandarasi hao kufanya kazi kwa weledi, uaminifu na kuzingatia maadili ya kazi ili kufanikisha malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi kwa haki na usawa.

Amesema Ofisi yake itafanya ukaguzi wa mara kwa mara kufuatilia utekelezaji wa mradi huo, huku akisisitiza kuepuka vitendo vya rushwa wakati wa kuwaunganisha wananchi na huduma ya umeme.

Mhe. Mtanda pia ametoa wito kwa wananchi kuwapokea vizuri wakandarasi hao na kuhakikisha wanapitia ngazi zote za Uongozi kuanzia Wilaya, Kata, Kijiji hadi Kitongoji ili kuwaelezea Viongozi kwa kina kuhusu mradi huo na vigezo vya uunganishaji.

Ameeleza kuwa nia ya Serikali ni kusogeza huduma karibu na wananchi, na pale mahitaji yatakapoongezeka, maboresho yatafanyika ili kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi wengi zaidi.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Miradi kutoka Ofisi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Seif Abdallah amesema Mkoa wa Mwanza umesaini jumla ya kandarasi mbili kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Amesema mradi huo utatekelezwa katika vitongoji 619 vya wilaya tano za Mkoa wa Mwanza kwa gharama ya shilingi bilioni 66.7 na unatarajiwa kuwanufaisha wateja 19,878.

Amefafanua kuwa White City International Contractors Ltd itahudumia vitongoji 306 katika Wilaya za Misungwi na Magu kwa gharama ya shilingi bilioni 32.7, huku Tibea Company Ltd ikitekeleza mradi katika vitongoji 313 vya Wilaya za Kwimba na Sengerema kwa gharama ya shilingi bilioni 33.7.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti