• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WANA MWANZA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI

Posted on: September 18th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WANA MWANZA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuendelea kuilinda na kuitunza amani tuliyonayo kwani imejengwa kwa muda murefu na kutokukubali kuruhusu watu wachache ambao hawaitakii mema nchi yetu kuja kuivuruga amani hiyo.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akizungumza na Waumini wa dini ya Kiislamu waliohudhuria katika sherehe za Maulid zilizofanyika katika Msikiti wa Raudhwa, Lumumba, Jijini Mwanza ambapo Maulid hiyo imeongozwa na Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally.

Mhe. Mtanda amesema Taifa haliwezi kujadili maendeleo kama hakuna misingi imara ya amani, hatuwezi kusonga mbele kama ndani hatuna amani, hivyo ni muhimu sana kuilinda na kuitetea amani hiyo ili tuweze kuwa na uwanda mpana wa kujadili na kuwaletea wananchi maendeleo.

"Mhe. Mufti ulitoa wito kwenye Baraza la Maulid kule Geita kukemea vitendo vya ukatili na uvunjifu wa amani, mimi nikuhakikishie Serikali ya Rais Samia na mimi nikiwa Mkuu wa Mkoa sitakubali kuona amani ya Wana Mwanza na Watanzania  inavunjwa" Amesema Mhe. Mtanda.

Aidha amesema yeye kama Mwenyekiti wa kamati ya Usalama Mkoa watafanya kazi usiku na mchana ili kuwalinda WanaMwanza na Wananchi wote wanaoingia na kutoka Mkoani humo.

Sambamba na hayo RC Mtanda ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa pindi wanapokutana na changamoto au tatizo lolote kwa  kupiga simu kwa serikali na wao watakuja na kutoa msaada.

"Hata ukipiga simu saa nane za usiku sisi tutakuja" Ameongeza RC Mtanda.

Naye Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally amesema amani sio kitu cha kuchezea tuendelee kuilinda amani yetu na kutokukubali kufanya jambo lolote bila ya kufikiri kwanza kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kupelekea majuto.

"Uislamu ni dini ya kufikiri na kufikiria kabla ya kufanya maamuzi kwa kila jambo hilo ndilo linalotakiwa na huo ndio uislamu thabiti".

Aidha Mhe. Mufti amewataka Waislamu hao kuungana na kumsaidia Mkuu wa Mkoa na yeye binafsi amesema anamjua sana ni mtu mzuri, ni mtu safi anaependa kuwatumikia wananchi wa dini zote japo yeye ni muislamu hivyo wamuunge mkono.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti