• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WANANCHI KUWAENZI MASHUJAA KWA KUWA WAZALENDO NA WAADILIFU

Posted on: July 25th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WANANCHI KUWAENZI MASHUJAA KWA KUWA WAZALENDO NA WAADILIFU


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi Mkoani humo kuwaenzi mashujaa walioipigania nchi wakati wa Uhuru kwa kuwa waadilifu, kufanya kazi kwa bidii na kuwa wazalendo kwa Taifa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo mapema leo  25 Julai 26, 2024 wakati akitoa salamu za Serikali na hotuba kwa wananchi katika maadhimisho ya siku ya Mashujaa, hafla iliyofanyika katika viwanja vya mzunguko wa ziro ziro jijini Mwanza.

"Tunapaswa kuwaenzi mashujaa kwa kuachana na matendo ya kujihusisha na rushwa, kupambana na dawa za kulevya na ujangili wa wanyamapori, kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuwa wazalendo kwa ujumla kwa Taifa." Mhe. Mtanda.

Aidha, Mhe. Mtanda amesema wananchi wana kila sababu ya kuwakumbuka mashujaa waliopoteza maisha wakiwa wanatetea na kupigania uhuru wa Tanzania na akatoa wito kwao kuwaombea dua na sala maalum.

"Historia ya Tanzania haiwezi kukamilika bila kuwataja mashujaa waliotumia mbinu na silaha za asili dhidi ya wakoloni waliotumia silaha wakati wa kulikomboa Taifa hili, twendeni tukapande mbegu ya utaifa, upendo, mshikamano ili kulinda mipaka na rasilimali za nchi yetu." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, ametoa wito kwa jamii kujiandaa na zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura zoezi litakaloanza Agosti 21, 2024 pamoja na kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu ili kuwapata viongozi wa Serikali ngazi ya mitaa, vijiji na Vitongoji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti