• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WANUFAIKA TASAF KUWEKA MALENGO KUPITIA FEDHA WANAZOPOKEA

Posted on: February 20th, 2025

RC MTANDA AWATAKA WANUFAIKA TASAF KUWEKA MALENGO KUPITIA FEDHA WANAZOPOKEA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wanufaika wanaopokea fedha za Mradi wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) kuweka malengo kupitia fedha wanazopata ili waweze kujikwamua na umaskini ambapo ndio lengo la msingi la mradi huo.

Mhe. Mtanda ametoa rai hiyo leo Februari 20, 2025 alipokuwa akizungumza na wanufaika wa mradi huo katika Kijiji cha Shigumulo Kata ya Mwang’halanga Wilayani Kwimba ambapo amewata wanufaika hao kujiwekea malengo ili waweze kuhitimu umaskini.

“Msaada huu ipo siku utakoma, ni lazima uwe na mipango, anzisha hata mradi wa kuku ambao utakusaidia kusomesha watoto, kuendesha familia na mwisho wa siku uweze kuhitimu kutoka kwenye mradi huu”.


Aidha Mkuu wa Mkoa amewapongeza Wanufaika hao ambao kundi kubwa alilokuatana nalo ni Wanawake na kuwataka kuwekeza katika kufanya kazi kwa bidii hata kupitia miradi ambayo TASAF imekuwa ikiibua ikilenga kuwawezesha Wanufaika hao pia kama vile ujenzi wa barabara, uchimbaji wa visima, mabweni au madaraja.

“Mtumie miradi hii kujikwamua na mbadilishe maisha yenu, fedha mnazozipata msiende kuzinywea pombe maana mradi utakwisha na wewe utakuwa umekwisha”.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ngw’ilabuzu Ludigija amewataka Wanufaika hao kuchukua wosia wa Mkuu wa Mkoa kwa kuwa aliyoyaeleza yote yana uhalisia na hawana budi kuyafuata.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti