• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZIHIMIZA HALMASHAURI KUONGEZA KASI UKUSANYAJI MAPATO

Posted on: June 7th, 2024

RC MTANDA AZIHIMIZA HALMASHAURI KUONGEZA KASI UKUSANYAJI MAPATO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amezitaka Halmashauri zote mkoani humo kuhakikisha wanafanya kazi ya usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuzisaidia Halmashauri zao ziweze kujiendesha na kuepukana na hali ya ukata.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo wakati akiongea na watumishi kwenye kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Misungwi leo tarehe 07 juni, 2024.

Sambamba na ukusanyaji mapato Mhe. Mtanda pia amewataka Watumishi wa Umma kuzipenda kazi zao kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii huku wakizingatia utoaji wa haki kwa wananchi wanaostahili.

"Kazi ndio msingi wa utu, tuzipende kazi zetu, wapo wanaochezea kazi zao kwa kuamua hata kulewa pombe lakini mimi naamini kwenye kazi kupata kipato na kujenga heshima." Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka watumishi wote kusimamia miradi ya maendeleo ili ikamilike kwa wakati na daima wawe wakweli kwenye utendaji wao  kwani hali hiyo itasaidia kuleta mshikamano utaoimarisha maelewano kazini.

"Mtumishi yeyote wa umma anayetoa huduma bora kwanza atapendwa na viongozi wake lakini pia atapendwa na wananchi, pokeeni wateja kwa utayari kwa kuwasikiliza." Amesema Mkuu wa Mkoa wakati akisisitiza suala la utoaji huduma bora.

Vilevile, amewataka watumishi kwenye idara zao kuhakikisha wanakua na mipango ya muda mfupi na mrefu na kuhakikisha wanaifuata na kuikamilisha ili kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi.

"Kufuata maadili ndio msingi mzuri wa kazi, tuwahi kazini na kuhakikisha tutekeleza majukumu yetu tena kwa wakati na sio kuwahi kazini na kushinda tunachezea simu hapana hiyo haikubaliki na tutachelewesha maendeleo kwa wananchi." Mkuu wa Mkoa.

Halikadhalika, ameipongeza halmashauri hiyo kwa kutekeleza vema maagizo ya viongozi kwa kusimamia ukusanyaji wa mapato hadi kukaribia kukusanya shilingi bilioni 4 tofauti na siku za nyuma ambapo walikua wanakusanya shilingi bilioni 2 pekee.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti