• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI, AWATAKA WATUMISHI KUWAJIBIKA KUTUMIKIA WANANCHI

Posted on: March 12th, 2025

RC MTANDA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI, AWATAKA WATUMISHI KUWAJIBIKA KUTUMIKIA WANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka watumishi Mkoani humo kufanya kazi kwa kujituma katika kuwatumikia wananchi na kutimiza wajibu bila kusubiri kuagizwa ili kuleta tija kwa Taifa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo tarehe 12 Machi, 2025 wakati akihutubia baraza la wafanyakazi la watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Rock City Mall, Ilemela.

Amesema, mtu akifanya kazi kwa kujituma atapata mshahara kihalali na kwa Mwenyezi Mungu atapata thawabu kutokana na ibada aliyoifanya kupitia kuwajibika bila kuchoka.

"Watu wengi wanadai haki lakini hawatimizi wajibu, hiyo sio sawa kwanza ni dhuluma ni lazima kila mmoja abadilike na kuchapa kazi ndipo afurahie mshahara anaoupokea kutoka Serikalini." Amesisitiza Mhe. Mtanda.

Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni lazima wawe na mwenendo wa maadili wakati wote kuanzia mavazi hadi lugha wanazozitoa kwa wananchi ni lazima ziwe na staha pamoja na kuacha tabia za kukopa pesa ovyo. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Halikadalika, amebainisha kuwa katika bajeti ya mwaka 2024/25 Ofisi yake imetumia Milioni 171.6 kulipa madeni kwa watumishi 53 na kupandisha vyeo kwa watumishi 102 na amewahakikishia watumishi kuwa Serikali inaendelea kuboresha maslahi ya watumishi.

Naye Mwenyekiti wa baraza hilo Bwana Balandya Elikana amesema baraza hilo lina manufaa makubwa ikiwemo kushirikisha wafanyakazi kutoa maoni na kupokea changamoto za watumishi na kuzifanyia kazi kupitia vikao mbalimbali vya kisheria hususan kwenye idara.

Awali, wajumbe wa baraza hilo walifanya uchaguzi ambapo bwana Gapchojiga Fabian ameshinda nafasi ya Katibu na Bi. Susan Ndunguru Katibu Msaidizi wa baraza hilo na mara moja viongozi hao wameanza miaka mitatu ya kutumikia nafasi zao kwa awamu ya pili mfululizo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti