• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZINDUA MRADI WA MAJI KABILA, WANANCHI ZAIDI YA 11, 000 KUNUFAIKA

Posted on: June 13th, 2024

RC MTANDA AZINDUA MRADI WA MAJI KABILA, WANANCHI ZAIDI YA 11, 000 KUNUFAIKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Juni 13, 2024 amezindua mradi wa maji wenye thamani ya zaidi ya  Tshs. Milioni 205 uliojengwa kwa ushirikiano baina ya SBL na RUWASA unaotarajiwa kunufaisha zaidi ya watu 11000 kutoka kwenye vijiji vya N'gwamagoli na Kabila.

Akizungumza na wananchi baada ya kuzindua mradi huo Mhe. Mtanda ameishukuru Kampuni ya Serengeti Breweries na AFRIcai kwa kutoa Tshs. 180,274,000 na kushirikiana na RUWASA (zaidi ya Bilioni 25) waliotekeleza mradi uliohusisha vituo vya kuchotea maji 13, mtandao wa mabomba KM 6.3 pamoja na tangi la lita 90,000.

"Mkoa wa Mwanza umetenga jumla ya Tshs. 146,315,299,905 katika mwaka 2023/24 - 2024/25 ambapo Wilaya ya Magu pekee imetengewa jumla ya Tshs. 17, 017,927,019 ili kukamilisha miradi 7 inayoendelea kutekelezwa." Amesema, Mkuu wa Mkoa.

RC Mtanda amefafanua kuwa ujenzi wa mradi huo muhimu kwa wananchi ni utekelezaji wa agenda ya Rais Samia katika kusudio lake la kumtua mama ndoo kichwani na utelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2025 inayoitaka Serikali kufikisha huduma ya maji vijijini kwa 85% au zaidi hadi kufikia 2025.

"Serengeti Broweries Limited imetumia zaidi ya Tshs. Bilioni 2.5 2023/24 kwenye uchangiaji wa miradi ya huduma kwa jamii ikiwa ni katika kuhakikisha inasaidia kuondoa adha ya upatikanaji wa maji safi na salama na kupambana na ukame unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi hususani vijijini." Mkurugenzi Mtendaji SBL, Dkt. Obinna Anyalebechi.

Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Joshua Nathari amewataka wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo ili lengo la kuongeza upatikanaji maji pamoja na kupunguza umbali na muda wa kufuata maji lidumu kwa muda mrefu na kusaidia kumaliza kero ya maji moja kwa moja.

Naye Meneja wa Wakala ya Maji vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mwanza Mhandisi Godfrey Sanga amesema Januari 2024 ujenzi wa mradi ulianza na Aprili 2024 umekamilika na kuna matarajio ya kufikisha asilimia 86 kutoka 71 za usambazaji maji vijijini kwa wananchi wa wilaya ya Magu.

"Tulikua tunasumbuka sana na huduma za maji lakini kwa sasa usumbufu wote umeisha kutokana na Rais Samia kutupendelea maana kwenye vitongoji vyetu vitano kati ya sita sasa tumepata naji safi tunaomba mtupelekee huduma hii kwenye kijiji hicho cha Ilambu." Mwenyekiti wa Kijiji cha Kabila, Mwajibu Boniface.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti