• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZITAKA NCHI WANACHAMA KUENDELEA KUDHIBITI UHALIFU UKANDA WA ZIWA VICTORIA

Posted on: May 21st, 2024

RC MTANDA AZITAKA NCHI WANACHAMA KUENDELEA KUDHIBITI UHALIFU UKANDA WA ZIWA VICTORIA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa nchi wanachama kuendelea na uthibiti na jitihada za kuondoa vitisho na uhalifu kuzunguka ziwa Victoria ili kuwaletea wananchi maendeleo kupitia shughuli za kiuchumi za uvuvi wanazofanya.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo mapema leo Jumanne 21 Mei, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha tatu cha kuimarisha usalama wa raia wanaofanya kazi katika ziwa Victoria kutoka Kenya, Uganda na Tanzania kilichoandaliwa na Shirika la Kimataifa linalihusika na masuala ya Uhamiaji (IOM).

"Wananchi wa Kenya, Uganda na Tanzania wanajivunia na uwepo wa ziwa Victoria lenye maji safi duniani na ni kitovu cha biashara na maisha kwa ujumla hivyo ni lazima tuhakikishe tunaandaa mipango ya kuhakikisha tunaondoa vitisho vyote vya kiusalama chini ya wadau wetu Serikali ya Marekani kwa kupitia mradi wa IOM", Mhe. Mtanda.

Amesema, ni wajibu wa Serikali za nchi zote tatu kuwa na mipango ya muda mfupi na mirefu ya kuhakikisha matukio mbalimbali yanayotishia amani kwa kuwa na uhalifu mipakani yanazuiliwa na kwamba kamisheni mbalimbali zinazofanya kazi kwenye bonde la ziwa hilo zinatakiwa kuwa msaada pia kwenye suala hilo nyeti.

Aidha, ametoa wito kwa wizara zinazohika na masuala ya usalama na undelezaji maliasili maji kutoka kwenye nchi wanachama kuweka mipango ya muda mrefu kupitia bajeti za nchi wanachama kuhakikisha utapoisha mradi wa IOM kunakua na muendelezo wa juhudi za uthibiti wa uhalifu kwenye mipaka ya ziwa Victoria.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti anayemaliza muda wake Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji kutoka Uganda Marcellino Kyamutetera amesema kwa kipindi chote akiwa kwenye uongozi amehakikisha nchi wanachama zinaongeza mahusiano ya kikanda katika kuhakikisha wanazuia kwa pamoja uhalifu wa mipakani.

Ndugu David Hofmeijer kutoka IOM Ofisi ya Tanzania amesema kikao kazi hicho kinalenga kuimarisha uhusiano na kukumbushana namna bora ya kuendelea kuboresha ulinzi kwenye mipaka ya nchi wanachana yanayolenga kukabiliana na uhalifu wa Kimataifa na tishio kwenye mipaka ya nchi wanachama.

Akitoa neno la ukaribisho, Kamishna Msaidizi kutoka Sekretarieti ya kupambana na usafirishaji wa binadamu (ATS) Ahmad Mwen-dadi ametumia wasaa huo kuwashukuru IOM na nchi wanachama kwa kuendelea kulinda mipaka ya nchi na kufanikisha malengo ya mradi huo.

Ameendelea kwa kusema bandari za nchi wanachama zote zipo salama ikiwa ni kutokana na ushirikiano mkubwa uliofanywa kwa pamoja kutoka 2023 ambao IOM imekua ikitoa mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa kutoka majeshi ya Uhamiaji, Polisi na wanamaji na kwamba mradi huo una msaada sana kwenye kuimarisha biashara na forodha.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti