• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA: BENKI ZISIJENGE MAFANIKIO BILA KUWAJALI WAFANYAKAZI

Posted on: January 29th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Januari 29, 2025 amefungua rasmi Mkutano wa Mwaka wa Mameneja wa Makao Makuu na Kanda wa Benki ya NMB, uliofanyika katika Ukumbi wa Malaika jijini Mwanza, na kusisitiza kuwa mafanikio ya taasisi za kifedha yanapaswa kuanza na ustawi wa wafanyakazi wake.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Mhe. Mtanda amesema ili benki iweze kufikia malengo yake makubwa ya kibiashara na kijamii ni lazima ijenge mahusiano imara kati ya menejimenti na watumishi wa ngazi zote.

Aidha, ameipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kutekeleza wajibu wake kwa jamii (CSR), akibainisha kuwa zaidi ya shilingi milioni 300 zilitolewa kusaidia jamii, ambapo zaidi ya shilingi milioni 60 zilitumika kuwasaidia wagonjwa wa saratani katika Hospitali ya Kanda Bugando.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda amezitaka taasisi za kifedha kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo mkoani Mwanza, akieleza kuwa mkoa huo unachangia asilimia 7.2 ya Pato la Taifa, ukiwa wa pili kitaifa baada ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Ameeleza kuwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza, ujenzi wa meli ya kisasa MV New Mwanza yenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 1,200, pamoja na uendelezaji wa reli ya SGR, utaifanya Mwanza kufikika kwa njia za anga, maji na reli na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi wa Kanda ya Ziwa.

Pia amesema Serikali imejenga Soko Kuu la Kisasa la Mjini Kati ili kuimarisha biashara za ndani na kupunguza utegemezi wa masoko ya nje ya mkoa, hususan Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Amehakikishia Benki ya NMB kuwa Serikali itaendelea kuiunga mkono, huku akiwahamasisha wananchi kutumia huduma za benki hiyo kutokana na mtandao wake mpana na uaminifu wake kwa jamii.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Bw. Philbert Mponzi amesema benki hiyo imekuwa ikiandaa mkutano huo kila mwaka kwa lengo la kufanya tathmini ya utendaji wa mwaka uliopita na kuweka mikakati ya utekelezaji kwa mwaka unaoendelea.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti