• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

Posted on: January 26th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesisitiza umuhimu wa kuwepo kwa dhamira ya dhati miongoni mwa wajumbe wa Kamati ya Maadhimisho ya Sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 Kitaifa kutoka Mkoa wa Rukwa, akibainisha kuwa dhamira ndiyo nguzo kuu ya mafanikio ya tukio lolote la kitaifa.

RC Mtanda ametoa msisitizo huo wakati wa mazungumzo na wajumbe hao waliotembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kujifunza na kupata uzoefu wa maandalizi ya Sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa zitakazofanyika Mkoani Rukwa tarehe 14 Oktoba, 2026.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bw. Msalika Robert Makungu amesema wajumbe wa kamati wamegawanyika katika makundi mawili, kundi moja likitembelea Mkoa wa Manyara na lingine likiongozwa na yeye mwenyewe likitembelea Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kujifunza namna ya kuandaa na kusimamia sherehe za Kuzima Mwenge wa Uhuru.

RC Mtanda amesema kuwa ili sherehe za kitaifa zifanikiwe ni lazima kuzingatia mambo muhimu ikiwemo ushiriki wa wananchi kwa wingi, upangaji wa bajeti ya kutosha, urembo wa tukio kupitia matangazo na sare zinazovutia pamoja na uwepo wa mfumo mzuri wa uratibu na uendeshaji wa shughuli.

Ameongeza kuwa vikao vya kupanga na ushirikishwaji wa wadau ni muhimu ili kuhakikisha kila mmoja anakuwa na uelewa wa majukumu yake.

Akihitimisha, amewahimiza wajumbe wa Kamati ya Maadhimisho ya Mwenge wa Uhuru 2026 Mkoa wa Rukwa kujitoa kwa moyo wote, akisisitiza kuwa kujituma hakufundishwi bali hutokana na dhamira binafsi na ushirikiano wa pamoja.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti