• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MWANZA AWATAKA WANANCHI KUENDELEA KUJISAJILI NA KUCHUKUA VITAMBULISHO VYA NIDA

Posted on: February 19th, 2024

RC MWANZA AWATAKA WANANCHI KUENDELEA KUJISAJILI NA KUCHUKUA VITAMBULISHO VYA NIDA


*Asisitiza weledi na Uzalendo kwa Mamlaka kwenye Utambuzi na Usajili wa wananchi*


*Atoa wito kwa wananchi kutunza vitambulisho na kuvitumia kwa mujibu wa sheria*


*Ametoa rai kwa Mamlaka hiyo kuandikisha makundi yenye Uhitaji Maalum*


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana leo Jumatatu Februari 19, 2024 amezindua ugawaji wa Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa wananchi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo na akatumia hafla hiyo kuwataka wananchi kufika kwenye vituo kujisajili na walivyojiandikisha kwenda wakachukue kadi zao kwani zipo tayari.

Balandya amebainisha kuwa tayari NIDA imekamilisha uzalishaji wa Vitambulisho kwa wananchi wapatao 716, 245 na kwamba vingi bado vipo kwenye Ofisi za Serikali za Mitaa na huku wananchi wakiwa na namba tu za kuwatambua jambo ambalo si sahihi hivyo ni wakati sasa wa kuvichukua kwa ajili ya rejea mbalimbali.

Balandya amesisitiza weledi na uzalendo kwa Mamlaka kwenye Utambuzi na Usajili wa wananchi ili waandikishwe wenye sifa kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo na kwamba kwenye utekelezaji wa zoezi hilo wasiliache kundi la watu wenye mahitaji maalum

Vilevile, Katibu Tawala ametoa wito kwa wananchi kutunza vitambulisho na kuvitumia kwa mujibu wa sheria na sio kwa matukio ya uvunjifu wa amani au kutenda makosa ya jinai.

Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mwanza Ndugu Daud Hashim Abdallah ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa hiyo kwani  kigezo kikubwa cha utambuzi na usajili ni kwa raia kuwa na Miaka 18 na kwamba Mamlaka hiyo imesajili asilimia 84 ya wenye sifa mkoani Mwanza na zoezi hilo ni endelevu.

Vilevile, ametaja changamoto kadhaa zinazowakabili Mamlaka hiyo kwenye zoezi hilo katika usajili na utambuzi wa wananchi ikiwemo muitikio mdogo wa wananchi katika kuchukua vitambulisho na kupelekea mlundikano wa vitambulisho kwenye ofisi za Serikali za mitaa na vijiji.

"Elimu kupitia vyombo vya habari imeendelea kutolewa na mamlaka kwenye redio na vyombo vingine kuhamasisha umma juu ya umuhimu wa kusajiliwa, kutambuliwa na kuchukua vitambulisho kwenye ofisi za Serikali za mitaa." Amesisitiza Ndugu Abdallah.

Aidha, bwana Abdalah ametaja pia changamoto za wananchi kujisajili zaidi ya mara moja na akatumia wasaa huo kuwataka kuwa na viambata muhimu kwa ajili ya usajili.

Jisajili, tukutambue tukutambulishe.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti