• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI IMETENGA BILIONI 4 KUJENGA HOSPITALI YA MKOA YA RUFAA UKEREWE: WAZIRI UMMY

Posted on: March 13th, 2024

SERIKALI IMETENGA BILIONI 4 KUJENGA HOSPITALI YA MKOA YA RUFAA UKEREWE: WAZIRI UMMY


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali imenuia kuondoa adha ya matibabu kwa wakazi wa Ukerewe na visiwa vya jirani kwa kutenga shs bilioni 4 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya mkoa ya Rufaa wilayani humo.

Akitoa taarifa fupi leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya afya na masuala ya ukimwi Waziri Ummy amebainisha kuwa Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kwa vitendo kuwaletea wananchi maendeleo ikiwemo kuiboresha sekta ya afya.

"Ndugu mwenyekiti wa kamati nimesimama hapa kutoa taarifa fupi ya Serikali, usumbufu wa matibabu na hata vifo kutokakana na jiographia ya Ukerewe sasa basi, naomba fedha zitakapofika Ofisi ya mkuu wa Mkoa mfanye usimamizi mzuri ili mradi huu wa ujenzi ukamilike kwa wakati na uwe na tija kwa wananchi", amesisitiza Mhe. Ummy

Kuhusu suala la upungufu wa watumishi zaidi ya elfu kumi kwenye sekta ya afya, Waziri Ummy ameziagiza Halmashauri zote mkoani humo kutumia mapato yao ya ndani kuwaajiri watumishi kwa mikataba wakati utaratibu wa ajira rasmi kutoka Serikali kuu  ukiendelea kufanyika.

Waziri Ummy pia amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa usimamiaji mzuri wa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu na kuhimiza utoaji wa elimu uzidi kuzingatiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema Mkoa huo umepokea jumla ya shs bilioni 48 ambazo ni gharama ya miradi ya afya na akaahidi kutaendelea kuisimamia ili iwe na tija kwa wananchi.

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya afya na masuala ya ukimwi ambaye pia ni Mbunge wa Maswa Mashariki Mhe. Stanslaus Nyongo amesema jukumu la kamati yake ni kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali zimetumika kwa malengo yaliyokusudiwa na pia kuishauri Serikali mpango sahihi wa kuwaletea maendeleo wananchi.


"Hospitali ya Sekou Toure tangu ilipoanza kuwa ya rufaa imezidi kupiga hatua kwa kutoa huduma bora na za kibingwa hasa baada ya Serikali kuzidi kuiboresha.

"Mhe Mwenyekiti wa kamati hospitali ya Sekou Toure sasa hivi tunatoa huduma za kusafisha damu pia Serikali imewasomesha Madaktari 17 tabibu za kibingwa lengo likiwa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi", Dkt. Bahati Msaki, Mganga Mfawidhi Sekou Toure.

Kamati hiyo ya Bunge itahitimisha ziara yake alhamisi ya hii kwa kutembelea Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya Bugando.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti