• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI INAKAMILISHA TARATIBU ZA KUMPATA MKANDARASI WA UJENZI WA BARABARA SENGEREMA-NYEHUNGE : RC MTANDA

Posted on: June 10th, 2024

SERIKALI INAKAMILISHA TARATIBU ZA KUMPATA MKANDARASI WA UJENZI WA BARABARA SENGEREMA-NYEHUNGE : RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi wa Wilaya ya Sengerema kuwa na subira wakati Serikali ikikamilisha taratibu za kumpata mkandarasi wa kujenga barabara ya Sengerema -Nyehunge kwa kiwango cha lami.

Amebainisha hayo leo Juni 10, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya zamani vilivyopo katikati ya mji huo ambapo ulikua wa muitikio mkubwa wa wananchi waliokua na kiu ya kumsikiliza kiongozi huyo wa Mkoa.

Amesema, awali Serikali ilitangaza kazi ya ujenzi wa barabara hiyo

yenye umbali wa takribani KM 50 na kwamba alipatikana mjenzi ambaye alitumia vyeti vya kughushi na kusababisha kupewa kazi wakati hakuwa na uwezo wa kutekeleza na kupelekea Serikali kuwaondoa na iko mbioni kuwachukulia hatua kwa udanganyifu.

"Serikali inayo nia ya dhati ya kujenga barabara ya Sengerema hadi Nyehunge kwa kiwango cha lami na sasa ipo kwenye mchakato wa kumpata mkandarasi mzuri wa kufanya mradi huo baada ya kumuondoa aliyepatikana awali ambaye amebainika kutokua na uwezo"

Vilevile, amewataka vijana kuchapa kazi na kuacha tabia ya kuketi kwenye vijiwe kwani wanasababisha kulirudisha nyuma Taifa kimaendeleo na badala yake wanapaswa kujibidiisha kujitafutia maendeleo kwa kufanya shughuli halali.

Vilevile, Mhe. Mtanda amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo ndani ya siku 14 kumlipa fidia Bi. Salome Kazungu ambaye mwaka 2017 Halmashauri ililitwaa eneo lake ili kulitumia kama eneo la kuzikana na endapo watashindwa kufanya hivyo atalirejesha kwa mmiliki huyo kwani hajapata haki yake kwa mujibu wa sheria ya ardhi na akatumia wasaa huo kuwataka sekta ya ardhi kushughulikia kero na migogoro.

Mhe. Hamis Tabasam, Mbunge wa Sengerema ametumia jukwaa hilo kumpongeza Rais Samia kwa kuwaletea miradi lukuki ya maendeleo huku akibanisha kuwa kwa sasa kuna shule za Msingi kwenye kila Kijiji na kwamba huduma za maji safi zimeimarika.

Aidha, Mhe. Tabasam amesema kuhusu mikopo kwa wananchi kutoka kwenye fungu la asilimia kumi kutoka fedha za mapato ya ndani tayari zimetengwa zaidi ya Shilingi milioni 300 ambazo zinasubiri utaratibu tu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ili zianze kukopeshwa kwa makundi husika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti