• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI YA UWEKEZAJI

Posted on: February 24th, 2025

SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI YA UWEKEZAJI


Serikali imedhamiria kuendelea kuweka mazingira wezeshi na rafiki kwa wawekezaji kuwekeza Mkoa wa Mwanza na Tanzania kiujumla ili kuchochea maendeleo na kukuza uchumi wa Mkoa na Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alipokuwa katika ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo katika kiwanda cha Ziwa Steel kilichopo Nyanguge Wilayani Magu.

Mkuu wa Mkoa amesema serikali itaendelea kuboresha miundombinu na kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji kwani Taifa likiwa na viwanda vingi inasaidia katika upatikanaji wa ajira, ukusanyi wa kodi na upatikanaji wa bidhaa kwa urahisi zitakazozalishwa kupitia wawekezaji hao.

“Kwa niaba ya Serikali ninaomba kuwapongeza Mkurugenzi na timu yako, lakini pia nitumie wasaa huu kuwakaribisha Wawekezaji katika Mkoa wetu wa Mwanza na Mwanza ni salama sana kwa uwekezaji”.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda amesema kilichomfurahisha zaidi ni kusikia kuwa kiwanda hicho kina mpango wa kuanza kutengeneza nashine za uchakataji wa dhahabu ambapo kwa ukanda huu ndio ukanda wa madini hayo.

“Mtakapoanza uzalishaji wa mashine hizo basi rai yangu ni kwamba msiwasahau pia wachenjuaji wadogo wa dhahabu”.

Kwa upande wake Afisa Utumishi wa Kiwanda hicho Bw. Philip Sylivanus amesema wanamshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuweka mazingira mazuri na kuvutia Wawekezaji, wamekuwa wakifanya kazi zao kwa urahisi hususani wakati wa kusafirisha malighafi na bidhaa zao.

Awali kabla ya kutembelea Kiwandani hapo Mkuu wa Mkoa pia alipata wasaa wa kutembelea na kukagua maendeleo katika Kiwanda Kipya cha Pepsi SBC kilichopo Nyakato Industrial Area, Wilayani Ilemela na kupongeza juhudi hizo za uwekezaji mkubwa uliofanywa na kiwanda hicho.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti