• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

Posted on: May 10th, 2025

SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana na Sekta binafsi Mkoani Mwanza na kusaidia upatikanaji wa huduma na mahitaji mbalimbali yanayotakiwa na Sekta hiyo.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo Mei 10, 2025 alipotembelea Kiwanda kipya cha kuzalisha vifaa vya migodini cha Rock Solution kilichopo Mayolwa, Usagara, Wilaya ya Misungwi na kumpongeza Mwekezaji kwa uwekezaji mkubwa alioufanya.

“Serikali itaendelea kushirikiana na wewe kwa sababu ni mzalendo lakini pia uwekezaji huu si kwa ajili ya familia yako lakini watu 300 wataajiriwa hapa”. Amesema.

"Na ndio maana serikali inapambana kuweka mazingira mazuri na wezeshi kwa Sekta binafsi kwa kuwa itaisaidia Serikali kupatikana kwa ajira rasmi na zile ambazo sio rasmi. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda ametoa wito kwa Uongozi wa Kiwanda hicho pamoja na Wawekezaji wengine wa Mkoa wa Mwanza kufika Ofisi za Serikali wanapokuwa na jambo au changamoto yoyote inayohitaji ufumbuzi.

“Nyie ni watu muhimu sana kwa uchumi na uzalishaji wa ajira za wananchi, milango ya Ofisi iko wazi wakati wowote mnakaribishwa”. Amesema Mkuu wa Mkoa.

Akisoma Taarifa ya Kiwanda hicho, Meneja wa Kiwanda cha Rock solution Bw. Fabian Mayenga amesema wameamua kufungua kiwanda hicho ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuimarisha sekta ya viwanda nchini na upatikanaji wa ajira.

Kiwanda hicho ambacho kimejizatiti katika uzalishaji wa vifaa vinavyokwenda kutumika migodini ikiwemo nyavu zinazotumika kuzuia maporomoko ya ardhi chini ya migodi, na sasa wapo katika hatua za ufungaji wa mitambo na mara watakapoanza uzalishaji wanatarajia kutoa ajira zaidi ya 300 za moja kwa moja na zisizopungua 500 zisizo za moja kwa moja.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti