• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

Posted on: May 10th, 2025

SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA


Serikali imedhamiria kununua mtambo maalum wa kusafisha ziwa victoria lililoathirika na gugumaji jipya ambalo limekuwa tishio kwa shughuli za uvuvi na usafirishaji kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 10, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alipokua akizungumza na Wananchi waliokuwa wakisubiri huduma ya usafiri wa kivuko katika eneo la Busisi Wilayani Misungwi.

Mkuu wa Mkoa amesema mpaka sasa fedha tayari zimeshatengwa na taratibu za manunuzi zimeshaanza na muda si mrefu mtambo huo utawasili na kazi hiyo ya uvunaji wa magugu maji itaanza mara moja.

“Kwanza tunamshukuru sana Mhe. Waziri Mkuu kutokana na kikao chake ndio tunaona matunda haya leo, lakini pia Mhe. Rais kwa kuidhinisha fedha”. Mhe. Mtanda.

Aidha, Mhe. Mtanda amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha Wafugaji wa Samaki kwa njia ya vizimba hawaathiriki na madhara ya magugu maji kwa kuwa serikali inafanya jitihada za makusudi kuhakikisha wanadhibiti hilo kwa teknolojia ya kisasa.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi hao kuwa na subira kutokana na changamoto ya usafirishaji kwa njia ya vivuko kwa kuwa sasa daraja la JPM liko hatua za umaliziaji na wakati wowote kuanzia sasa litazinduliwa rasmi.

“Mwenye macho haambiwi tazama, sasa daraja linakamilika tuendelee kuvuta subira, siku si nyingi changamoto hii itakua imekwisha kabisa”. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa amembatana na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Cyprian Luhemeja ambaye amesema ushirikiano uimarishwe kazi ifanywe kwa pamoja baina ya Wataalamu wa Kisekta, Wavuvi, pamoja na Wafugaji wa vizimba ili ziwa libaki salama na matokea mazuri na ya muda mrefu yapatikane.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti