• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Serikali Yaahidi kuendelea kuboresha Mazingira ya kazi kwa Wauguzi nchini

Posted on: May 12th, 2023

**Serikali yaahidi kuendelea kuboresha mazingira ya Wauguzi nchini.*


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ameahidi Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa Wauguzi nchini kutokana na kutambua mchango wao katika Sekta ya afya nchini.

Akizungumza kwa niaba yake katika hafla ya ufungaji wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Wauguzi nchini TANNA kwenye ukumbi wa Malaika Resort, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Ndg.Balandya Elikana amesema Serikali imekuwa ikiweka kipaumbele cha bajeti Sekta ya afya kwa kuboresha huduma zote kwa ujumla yakiwemo mazingira ya Wauguzi.

Amesema siyo rahisi kutatua changamoto zote kwa mara moja zinazowakabili kada hiyo,lakini kadiri bajeti inaporuhusu kipaumbele kitawekwa lengo likiwa kuboresha kwa ujumla Sekta ya afya nchini

"Nimesikia katika risala yenu baadhi ya changamoto zinazowakabili,yale ya ngazi ya Mkoa tutayafanyia kazi na yale yaliyo juu ya uwezo wetu yatafikishwa TAMISEMI ili yapatiwe ufumbuzi",amesema Mtendaji huyo wa Mkoa

Aidha amewakumbusha Wauguzi hao Mkutano huo wa siku tano uliofanyika Mwanza umeambatana na makongamano mbalimbali ya Kisayansi,wayatumie kama chachu ya kuongeza ufanisi wa kazi watakaporudi makazini.

"Kipaumbele chetu sasa ni ubora wa huduma,wakati Serikali ikizidi kuwekeza katika Sekta ya afya,Wauguzi nao wanaendelea kupatiwa mafunzo mbalimbali yakilenga staha,heshima na maadili ili wateja waendelee kupatiwa huduma bora,hadi sasa Wauguzi 2500 wamepatiwa mafunzo hayo",Saturin Mwanangwa,Mkurugenzi wa huduma na uuguzi Wizara ya Afya.

"Licha ya mazingira yenye changamoto kwa Kada hii ikiwemo kutoa huduma kwa wateja wengi,lakini tutaendelea kusimamia kiapo chetu cha kuwa watumishi wenye weledi,"Alexander Baluya,Rais wa TANNA.

Ufungaji huo umekwenda pamoja na Maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani inayofanyika kila Mei 12 yaliyokwenda pamoja na kurudia kiapo kwa Wauguzi hao akikumbukwa mwanzilishi wa huduma za uuguzi na ukunga Duniani,Florence Nightingale raia kutoka Italia.

Mara baada ya kutoka katika ufungaji huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amemtaka Mkandarasi aliyepewa kazi ya ujenzi wa Kituo cha Mawasiliano na Uokozi Ziwa Victoria chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC kumaliza mradi huo kwa wakati na kuzingatia ubora na thamani kutokana na majanga ya ajali yanayotokea mara kwa mara Ziwani humo.

Mkandarasi Obuntu kutoka Uganda anatarajiwa kukamilisha ujenzi huo ndani ya mwaka mmoja.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti