• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

Posted on: May 1st, 2025

SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA


Serikali mkoani Mwanza imesema Katika kipindi cha mwaka 2023/2024 na 2024/2025 Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri zake nane zimepata mafanikio makubwa katika kuhakikisha kwamba masuala ambayo ni kero kubwa kwa watumishi yamefanyiwa kazi kwa kiasi kikubwa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika Kimkoa katika Viwanja vya KWIDECO Wilayani Kwimba ambapo amesema Serikali imelipa watumishi 3,556 fedha za malimbikizo ya mishahara (Salary Arreas) yenye jumla ya shilingi 6,896,355,330/= na Watumishi wapya 831 wameajiriwa ili kupunguzia mzigo kwa watumishi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema Serikali imelipa madai ya watumishi 4,015 yasiyo ya mshahara (mfano likizo, matibabu uhamisho n.k) yenye kiasi cha Shilingi 3,283,016,595,486/=.

“Si hayo tu bali pia Watumishi 9,829 wa kada mbalimbali wamepandishwa madaraja (vyeo) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na watumishi 601 wamebadilishiwa kada (Recategorization) kwa mwaka wa fedha 2023/2024”.

Kadhalika Watumishi wameendelea kupewa fursa za kujiendeleza ambapo hadi kufikia mwezi Aprili, 2025 jumla ya watumishi 528 wapo masomoni katika Vyuo mbalimbali. Watumishi 1,352 wameajiriwa katika sekta mbalimbali ndani ya Mkoa wa Mwanza. Amesema Mhe. Mtanda akiendelea kuelezea mafanikio hayo.

Mkuu wa Mkoa ameendelea kwa kusema Utekelezaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma (PEPMIS) kwa mwaka wa fedha 2024/2025, umefikia asilimia 59.72 huku Mfumo huo ukiwa na lengo la kuimarisha uwajibikaji na utendaji kazi unaojali matokeo katika Utumishi wa Umma ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Kuhusu suala ya Ajira kwa Vijana Mkuu wa Mkoa amesema Jumla vikundi 37 vya vijana hadi sasa vimewezeshwa miundombinu ili kufuga Samaki kwenye vizimba 161 ndani ya ziwa Victoria hivyo

kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana wa Mkoa wa Mwanza.

“Miradi ya Kimkakati imezalisha ajira mbalimbali kama vile Ujenzi wa madarasa na ujenzi wa miundombinu mingine ya Utawala, Elimu na Afya ulizalisha ajira 15,855, Ujenzi wa Meli Mpya ya MV Mwanza Hapa Kazi tu umezalisha ajira 1,000, Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR umezalisha ajira 3,075, Ujenzi wa daraja la JPM umezalisha ajira 1,875 Huku Ajira 2,758 zimezalishwa kupitia fedha za Mfuko wa Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulememavu.”.

Mkuu wa Mkoa amesema kwa kufafanua mafanikio hayo ni kuwafanya Wafanyakazi hao waweze kupata picha halisi ya mafanikio makubwa na ya kupigiwa mfano yaliyopatikana kwenye upande wa watumishi katika Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti