• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SHULE MPYA YA GHOROFA KATA YA MHANDU KUMALIZA MSONGAMANO WANAFUNZI DARASANI

Posted on: January 29th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 29 Januari, 2026 amekagua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa shule mpya ya Sekondari kwa mfumo wa ghorofa mtaa wa Kasota, kata ya Mhandu Wilayani Nyamagana.

Akizungumza na wananchi kwenye hafla hiyo Mhe. Mtanda ameipongeza serikali kwa kutoa fedha na Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa maendeleo ya kasi katika sekta ya elimu na kwamba kuanzia mwaka 2021 hadi sasa kumekua na ongezeko la shule za sekondari 58 kutokana na juhudi zao.

Aidha, ameiagiza Halmashauri hiyo kutoa fedha Tshs. Milioni 200 na kusimamia kwa kasi ukamilishaji wa ujenzi wa shule hiyo hadi kufikia mwezi desemba mwaka huu ili mapema mwezi januari mwakani wanafunzi waanze kusoma katika madarasa ya shule hiyo mpya na kusaidia kuondoa msongamano kwenye shule mama.

Halikadhalika, amewataka MWAUWASA na TANESCO kuhakikisha wanafanikisha huduma za Maji na Umeme kwenye shule hiyo mpya ili kuongeza kasi ya ujenzi na pia kwenda sambamba na ujenzi wa miundombinu mara ujenzi utakapokamilika wanafunzi waanze kuyatumia bila kusubiri huduma za msingi.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema shule hiyo itakapokamilika itachukua wanafunzi 1620 na itasaidia Kata hiyo kuwa na shule mbili za sekondari na kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani pamoja na kupunguza umbali kwa wanafunzi kwenda Mhandu sekondari.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mhandu Warioba Marato amesema Mwezi Juni 2025 Serikali ilitoa Tshs. Milioni 584.2 kwa ajili ya kujenga Shule ya sekondari ya kawaida katika kata hiyo lakini kutokana na ongezeko la wanafunzi kuwa kubwa halmashauri iliamua kujenga kwa mfumo wa ghorofa.

Mwalimu Marato ameongeza kuwa mnamo Mei 2025 kibali kilitolewa na kuanza rasmi kwa ujenzi wa shule hiyo kwa mfumo wa ghorofa katika mtaa wa Kasota na hadi kukamilika wanahitaji nyongeza ya Tshs. Bilioni 1.56 ambapo sasa ujenzi umefikia 45%.

Halmashauri ya wilaya ya Nyamagana kwa mwaka 2026 wanafunzi 13609 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza na mpaka sasa wanafunzi 10195 wameripoti shuleni.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti