• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SUALA LA UPANDAJI MITI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA LIWE ENDELEVU:RC MTANDA

Posted on: December 9th, 2024

SUALA LA UPANDAJI MITI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA LIWE ENDELEVU:RC MTANDA


Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mh:Christopher Ngubiagai ametaka kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake kwa kutambua umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ili kupambana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoendelea kuleta madhara makubwa duniani kwa sasa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati wa maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru yaliyofanyika ki Mkoa wilayani Ilemela kwenye viwanja vya Halmashauri,comrade Ngubiagai amebainisha Dunia hivi sasa inashuhudia maafa makubwa ya mafuriko na kuangamiza maisha ya watu hii ni kutokana na athari za mazingira.

“..Uhuru ni haki ya msingi ya kila mtu au Taifa kuamua kufanya mambo bila kuingiliwa na mtu yoyote ki maamuzi,sisi watanzania hatuna budi kuendelea kuuenzi Uhuru wetu kwa vitendo likiwemo suala la utunzaji mazingira” Amesema Mkuu huyo wa wilaya akimnukuu hayati baba wa Taifa la Tanzania Mwl.Julius Kambarage Nyerere

Mhe:Ngubiagai ameongeza kuwa pamoja na shughuli mbalimbali ambazo zinafanyika katika maadhimisho hayo ni muhimu kuwaenzi waasisi wa Taifa kwa kuzingatia misingi ya uhuru ambayo inajumuisha umoja,usawa,uwajibikaji,kujitegemea na haki za binadamu ili kuleta maendeleo kwa kasi.

“..Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayoendelea nayo ya kuleta maendeleo,kipindi cha uhuru mkoa wa Mwanza ulikuwa na shule 5 tu leo tuna jumla ya shule 332 na nyingine zinaendelea kujengwa."

Aidha Afisa usalama mstaafu wa mkoa wa Mwanza Dkt.Jacob Mutashi ametoa mada kuhusu amani wakati wa kongamano lililojikita zaidi katika masuala ya Uhuru wa Tanzania Bara, amesema nchi hiyo ilipata uhuru wake kwa njia ya amani bila kumwaga damu na kwamba nchi iliongozwa kwa kufuata misingi ya amani ,umoja na uadilifu bila kujali dini wala makabila ya mwananchi wake.

“.. Hatuna budi kuilinda tunu ya Taifa letu ambayo ni amani..” amesema Dkt.Mutashi

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilemela mstaafu Dkt.Leonard Masale amesema Tanzania Bara inatimiza miaka 63 ya Jamhuri huku akifafanua maana jamhuri kuwa ni jamii huru

Maadhimisho hayo yaliyokwenda pamoja na kongamano la miaka 63 ya Uhuru na shughuli ya upandaji miti yamepambwa na kauli mbiu isemayo "Uongozi madhubuti na ushirikishwaji wa wananchi ni msingi wa maendeleo yetu."

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti