• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

TEMESA watakiwa kuboresha huduma ili kujenga imani kwa wateja wao

Posted on: May 24th, 2023

**TEMESA watakiwa kuboresha huduma ili kujenga imani kwa wateja wao*


Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wametakiwa kubadilika na kuboresha huduma zao kwa wateja ili kuwa mfano wa utoaji wa huduma bora.

Akifungua Warsha ya Wadau wa TEMESA leo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ndg.Joachim Otaru amesema kwa muda mrefu Taasisi hiyo imekuwa ikilalamikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo huduma duni, kutokuwa waaminifu wa vipuri,na ucheleweshaji wa matengenezo ya magari.

Otaru amebainisha baada ya Serikali ya awamu ya Sita kuanza kuiboresha Taasisi hiyo kuanzia ngazi ya uongozi, fedha na vifaa,sasa ni jukumu la TEMESA kutoa huduma zenye tija.

" Kabla sijaingia kufungua Warsha hii nimeoneshwa hapo aina ya huduma mnazotoa kwenye magari na mitambo mkiwa na vifaa vya kisasa pamoja na gari maalum la utoaji wa huduma na nimeambiwa vifaa hivyo vipo nchi nzima,hongereni sasa onesheni ubora wenu," amesema Otaru.

Ameongeza kuwa wateja wote wanaodaiwa na TEMESA wafanye hima kulipa madeni yote ambapo Mkoa wa Mwanza una wadai wateja wake deni la zaidi ya Shs Bilioni 1.45,fedha ambazo ni nyingi zinazochongia kurudisha nyuma utoaji wa huduma.

"Tumezifanyia kazi changomoto nyingi zilizokuwa zinatukabili ambapo Mafundi wetu wanaendelea kupatiwa mafunzo kwenye vyuo mbalimbali,Karakana zetu zote 13 nchini tumefunga camera za kisasa za kubaini aina yoyote ya wizi wa vipuri,kwa kifupi utoaji wa huduma zetu umekuwa wa kiwango kizuri tofauti na hapo awali," Mhandisi Hussein Karonda,Kaimu Mtendaji Mkuu,TEMESA.

"Kituo chetu cha Mwanza licha ya kuwadai wateja wetu fedha nyingi lakini tunashukuru Serikali imezidi kutuwezesha kila mwaka,mfano mzuri ni vifaa hivi na gari maalum lenye gharama ya Shs Milioni 700 vinavyotupa ari ya utoaji wa huduma bora kwa magari na mitambo ya Serikali," Mhandisi Gilly Gabriel Chacha,Meneja wa TEMESA Mwanza.

Aidha baadhi ya Wadau wa Taasisi hiyo wamepatiwa hati maalum kutokana na kutambua mchango wao akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima na baadhi ya Wazabuni wa Vipuri wanaoendelea kushirikiana na TEMESA kutoa huduma kwa wateja.

Warsha hiyo yenye lengo la kuwasikiliza Wadau kuhusiana na changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi imewashirikisha Makatibu Tawala wa Wilaya zote za Mwanza,Mameneja wa Mikoa wa TEMESA,Wakurugenzi wa Halmashauri za Mwanza pamoja na Wazabuni wa Vipuri.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti