• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

TRA MWANZA YATOA MAFUNZO YA MFUMO JUMUISHI WA KODI ZA NDANI KWA WAFANYABIASHARA

Posted on: January 28th, 2026

Katika kuimarisha na kurahisisha shughuli za ukusanyaji wa mapato nchini, Mamlaka ya Mapato (TRA) imeanzisha Mfumo jumuishi wa Kodi za ndani ambao unatarajiwa kuanza kutumika ifikapo Februari 09, 2026 kote nchini na TRA Mwanza inatoa mafunzo kwa wafanyabiashara ili kujengewa uwezo.

Akifungua Mafunzo hayo katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana ameipongeza Mamlaka hiyo kuingia kwenye dunia ya kidigiti ambapo itaongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato kwani mfanyabiashara hatokwenda katika ofisi za TRA kufuata huduma.

“Nawapongeza sana TRA kwa kuja na wazo ambalo linaenda sambamba na dira ya serikali ya kutumia TEHAMA kusogeza na kurahisisha huduma za kikodi kwa wafanyabishara nchini.” Amesema Katibu Tawala.

Aidha, amewataka TRA kuhakikisha kabla ya kutekeleza mfumo huo wawafikie wafanyabiara kwa umakini na kuwapitisha katika moduli zote ili kusiwe na changamoto zitokanazo na ugumu wa mfumo.

“Ninawashukuru wafanyabiashara wa Mwanza kwa kuwa walipa kodi wazuri na natoa wito kwenu tuendelee hivyohivyo kwani kodi ndizo zinaipa fursa serikali kufanya miradi ya maendeleo ya jamii kama tulivyoona Daraja la JPM pamoja na Meli ya Kisasa vilivyotekelezwa na kodi zetu na sasa zinakwenda kuinua uchumi wetu.” Ndugu Balandya.

Akitoa utangulizi, Meneja wa TRA Mkoa wa Mwanza Bw. Faustine Mdesa amesema Kikao hicho cha siku tatu ni mahususi kwa wafanyabiashara kupatiwa mafunzo ya mfumo Jumuishi wa Kodi za ndani ambao unatarajiwa kuanza kufanya kazi ifikapo februari 28, 2026 kote nchini.

Amebainisha kuwa wafanyabiashara hao watapitishwa kwenye moduli 17 za zinazojumuisha namna ya Usajili, Ulipaji na ufuatiliaji wa masuala ya kikodi ambayo kwa ujumla yatampa fursa mfanyabiashara kumaliza masuala yote ya kikodi ndani ya mfumo pasipo kwenda kwenye ofisi za TRA.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti