• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tuhakikishe Maafisa Utumishi Wanatekeleza Majukumu yao bila Kikwazo: Waziri Simbachawene

Posted on: August 3rd, 2023

Tuhakikishe Maafisa Utumishi Wanatekeleza Majukumu yao bila Kikwazo: Waziri Simbachawene*


Waziri wa Nchi, Ofis ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe. George Simbachawene amewataka waajiri nchini kuhakikisha wanawajengea uwezo Maafisa utumishi ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Waziri Simbachawene ametoa agizo hilo mapema leo tarehe 03, Agosti 2023 wakati akizungumza na watumishi kwenye mapokezi yake alipowasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya ziara ya kikazi ya Siku mbili.

Amesema, katika uboreshaji wa sekta za utumishi na Rasilimali watu idara hiyo ina majukumu mazito kama ufuatiliaji wa nidhamu, kupandishwa vyeo na uhuishaji wa taarifa za kiutumishi kwenye mfumo ambapo kwa pamoja zinahitaji umakini na weledi.

"Tuhakikishe Maafisa utumishi wanatekeleza Majukumu yao bila kikwazo ili waweze kuwa na utulivu wa utendaji kazi wenye weledi wakati wote katika kukuza sekta hii muhimu." Amesisitiza Mhe. Simbachawene.

Vilevile, Mhe. Waziri amewaagiza Maafisa utumishi kuhakikisha kujaza taarifa za watumishi kwenye mfumo wa utumishi ili kurahisisha utendaji kama upandishaji wa madaraja na uwajibishaji wa masuala mbalimbali ya kinidhamu.

Akimkaribisha Mhe. Waziri, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amempongeza kwa utendaji wake mahiri unaodhihirisha dhamira ya Serikali katika kuboresha sekta ya Utumishi na utawala bora nchini na amemuahidi ushirikino katika kipindi chote cha ziara yake mkoani humo.

"Mhe. Waziri sisi tunakushukuru sana kwa kutupa upendeleo maana Mkoa wa Mwanza umekua Mkoa wako wa kwanza kufanya ziara ya kiutumishi na ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na wizara yako maana yake sasa upo 'Site'." CPA Makalla.

Waziri Simbachawene yupo Mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja na masuala ya kiutumishi anatarajiwa kukagua miradi inayotekelezwa na Mfuko wa kunusuru kaya masikini -TASAF katika wilaya za Kwimba na Misungwi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti