• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

TULITUMIE JUKWAA LA UMISSETA NA UMITASHUMTA KUPATA HAZINA YA WANAMICHEZO WA TAIFA:RAS BALANDYA

Posted on: June 10th, 2024

TULITUMIE JUKWAA LA UMISSETA NA UMITASHUMTA KUPATA HAZINA YA WANAMICHEZO WA TAIFA:RAS BALANDYA


Mashindano ya Michezo ya Umoja wa Shule za Sekondari UMISSETA na Umoja wa Shule za Msingi UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Mwanza yamefungwa leo rasmi na rai kutolewa Jukwaa hilo litumike vizuri kupata hazina ya wanamichezo wa Taifa.

Akifunga mashindano hayo leo Alasiri kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Nsumba kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu Bw.Daniel Machunda amesema wanamichezo nyota wanaotamba hivi sasa Duniani wameanzia ngazi kama hizi na kupata muendelezo mzuri,hivyo hatuna budi kuvibaini vipaji vinavyoonekana na kuviwekea mkakati maalum wa kuviendeleza.

"Kwa muda mfupi nimekaa hapa nimeona uwezo mzuri wa vijana wetu hasa katika sanaa za ngoma na kwaya,ni jambo la kujivunia sana,hii ni hazina nzuri ya Taifa tunaishukuru Serikali kwa kuweka mashindano haya kila mwaka"amesisitiza Machunda.

Aidha amewataka wanamichezo wote bora waliopata nafasi ya uteuzi kwenda kushiriki mashindano ngazi ya Taifa kutanguliza nidhamu ambayo ndiyo silaha ya mafanikio.

"Sasa hivi wanamichezo ndiyo wanalipwa fedha nyingi Duniani,lakini hadi kufikia hatua hiyo nidhamu ndiyo silaha ya pekee ni lazima mjitambue,muwe wasikivu kwa walimu wenu,ongezeni bidii na kuzingatia maelekezo yote ya msingi huo ndiyo msingi wa kupata mafanikio,"Machunda

Akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Afisa Michezo Mkoa wa Mwanza,James William amebainisha mashindano hayo yameshirikisha michezo 9 ukiwemo soka kwa wavulana na wasichana,mpira wa kengele kwa albino na wenye ulemavu wa macho,mpira wa kikapu,pete,mezani,wavu na mikono kwa wasichana na wavulana pia imeshirikishwa sanaa za jukwaani ambazo ni kwaya,ngoma,mziki wa kizazi kipya(Singeli) na uchekeshaji.

"Ndugu mgeni rasmi tumepata jumla ya wanamichezo bora 120 na tumeongeza 40 tutafanya mchujo ili kuwapata 120 watakaokwenda kushiriki ngazi ya Taifa huko mkoani Tabora kuanzia Juni 17 hadi 27 mwaka huu",Afisa Michezo.


Katika mashindano ya ngazi ya Mkoa mwaka huu mshindi wa jumla ni Wilaya ya Nyamagana ikufuatiwa na jirani zao Ilemela.

Kwa miaka minne mfululizo Mkoa wa Mwanza umeshika nafasi ya pili Kitaifa kwenye Mashindano ya Umissseta

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti