• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tumieni fursa za Ufugaji na Kilimo kujihakikishia vipato vyenu baada ya kustaafu: RAS Balandya

Posted on: August 4th, 2023

Tumieni fursa za Ufugaji na Kilimo kujihakikishia vipato vyenu baada ya kustaafu: RAS Balandya


Umoja wa wazee Mkoani Mwanza, UWAMKOMWA umekumbushwa kuutumia umoja huo katika kuelimishana kuhusu fursa zilizopo hivi sasa katika sekta ya kilimo na ufugaji ambazo zitakuwa mkombozi wa vipato vyao baada kustaafu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana ametoa rai hiyo leo wakati wa mkutano na umoja wa wazee hao uliofanyika kwenye ukumbi wa jengo la Nyanza kwa lengo la kujitambulisha rasmi, Balandya amelitumia jukwaa hilo kuwafahamisha wapo baadhi ya wazee baada ya kustaafu wanapata shaka na hatma ya maisha yao wakati zipo fursa za kuendesha maisha yao bila kutumia nguvu nyingi kama alivyokuwa kazini.

"Ndugu Mwenyekiti wa umoja huu mzee wangu Masalakulangwa hapa nimekuja na timu ya wataalamu wa kilimo na mifugo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambao watawasaidia kuwaelimisha na kuwafafanulia masuala mbalimbali ambayo yalikuwa ni changamoto kwenu,Serikali imetenga fedha nyingi kwa lengo la sekta hiyo sasa iwe na tija na siyo kama zamani kutumia uzoefu tu,"amefafanua Mtendaji huyo wa Mkoa.

Balandya amebainisha sasa hivi kwenye shamba la mifugo Mabuki kuna elimu inaendelea kutolewa namna ya ufugaji wa Ng'ombe kitaalamu kwa muda mfupi ambaye anakuja kutoa lita nyingi za maziwa na mwenye uzito wa kutosha wa kulimudu soko la nyama.

"Nawasihi sana wazee wangu tufike hapo Mabuki ili mfaidike na mageuzi haya kwenye kilimo na kuondokana na ufugaji wa ng'ombe wengi wasio na tija,"Balandya.

Mwenyekiti wa umoja wa wazee Mwanza,Charles Masalakulangwa amesema lengo la umoja huo  ni kuwa na Wazee wenye busara na maadili mema watakao weza kuishauri vizuri Serikali masuala mbalimbali.

"Tuchangamkie pia Zabuni za kufanya usafi zinazotolewa na Halmashauri zetu,undeni vikundi msajili ili mjihamikishie hizo kazi ambazo zitawafanya msiwe watu wa kukaa na kusubiri siku za malipo ya Pensheni na badala yake zitawaimarishia pia afya zenu kwa kujishughulisha,"Janeth Shishila,Afisa Maendeleo ya Jamii

"Sasa hivi upo ufugaji wa kisasa wa samaki kwenye vizimba mnaweza kuunda umoja wenu au mtu mmoja mmoja na kujikuta mnapata faida kwa muda mfupi,nawakaribisha pia kwenye maonesho ya Nananane mje kupata ufahamu wa fursa mbalimbali zitakazo kuwa na faida kwenu,"Emil Kasagara,Katibu Tawala Msaidizi,Uchumi na Uzalishaji.

"Mnada wa mifugo wa Nyamatala uliopo Wilayani Misungwi haujafungwa kama inavyodhaniwa bali shughuli zake zimepungua siyo kama zamani kutokana na wafugaji wengi kuleta mifugo yao nje ya muda,lakini bado ni mnada muhimu na Serikali inaendelea kutoza ushuru na kuwapima ng'ombe wote kabla ya kumfikia mlaji,"Peter Kasele,Afisa Mifugo.

Umoja wa wazee Mkoani Mwanza UWAMKOMWA ulioanzishwa rasmi Juni 15,2022  una wanachana hai 37 kutoka Wilaya zote 7 za Mkoa huo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti