• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tumieni Jukwaa hili la mkutano wenu mkuu ili mje na maboresho zaidi katika sekta ya elimu nchini: Naibu Waziri Ndejembi

Posted on: December 15th, 2023

Tumieni Jukwaa hili la mkutano wenu mkuu ili mje na maboresho zaidi katika sekta ya elimu nchini: Naibu Waziri Ndejembi


Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi Mhe. Deogratius Ndejembi ameutaka umoja wa walimu wa shule za Sekondari nchini TAHOSSA kuutumia mkutano wao mkuu wa 18 unaofanyika Mkoani Mwanza kama jukwaa la kuleta mageuzi chanya katika sekta ya elimu nchini.

Mh.Ndejembi ametoa rai hiyo leo wakati akifungua mkutano huo kwenye ukumbi wa Malaika Beach Resort, amebainisha umoja huo ni chombo muhimu katika kuleta maendeleo hivyo yote yatakayojadiliwa kwenye mkutano huo yawe na tija kwa Taifa letu.

"Rais wetu ameonesha nia ya dhati ya kupigania maendeleo ya nchi yetu kwa kuboresha sekta ya elimu, wote ni mashuhuda wa fedha za Uvico19 zilivyo jenga madarasa bora nchini nzima, ni wajibu wetu sisi kumuunga mkono kwa vitendo ili kutimiza ndoto yake ya kuona Taifa linazidi kustawi kwa viwango bora vya elimu kwa wanafunzi," Naibu Waziri.

Amewahimiza wakuu hao wa shule kuendelea kuwa wafanyakazi wa mfano kama walivyoonesha wakati wa ujenzi wa madarasa yaliyokamilika kwa wakati, ubora unaokwenda na thamani ya fedha na weledi wa matumizi ya fedha zilizo kusudiwa.

Aidha katika Mkutano huo Mhe. Ndejembi alitoa maamuzi ya kiwanja cha TAHOSSA kilichopo eneo la Ihumwa, Dodoma kilicholengwa kama kitega uchumi chao, warejeshewe mara moja baada ya kupewa taasisi ya MKURABITA ambayo tayari imefutwa, alipompigia simu ya hadharani Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na kumpa maelekezo hayo.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi wa mkutano huo Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza,Ndg.Balandya Elikana amesema mwaka  2023-24 wamepokea jumla ya Shs bilioni 89.7 kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika sekta ya elimu hali iliyochangia kuwa na madarasa bora na wanafunzi kusomea katika mazingira rafiki yasiyo na msongamano.

"Ndugu Naibu Waziri Ofisi ya mkuu wa mkoa imesimama imara kuhakikisha miradi yote iliyokusudiwa katika sekta ya elimu inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaokwenda na thamani ya fedha,"amesema mtendaji huyo wa mkoa mbele ya wakuu wa shule za sekondari.

Rais wa TAHOSSA Dennis Otieno amesema katika siku tatu za mkutano wao watajadili mambo mbalimbali ya kuboresha elimu nchini ikiwemo kuzitambua na kuzipa zawadi maalum shule zinazofanya vizuri na zile zisizofanya vizuri kuona zinakabiliwa na changamoto gani ili kupata ufumbuzi.

Mkutano huo unatarajiwa kufungwa Disemba 17,2023 na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi Mhe.Mohamed Mchengerwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti