• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Uhusiano baina ya Tanzania kichocheo cha kuinua uchumi-Balozi Chen

Posted on: September 9th, 2023

Uhusiano baina ya Tanzania kichocheo cha kuinua uchumi-Balozi Chen


Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania Mhe.Chen Mingjian amesema Tanzania na China zitaendelea kufaidika na uhusiano mzuri ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere na Mao Tsetung katika kuinua uchumi wa nchi hizo kupitia nyanja mbalimbali.

Balozi Chen amezungumza hayo leo Mkoani Mwanza akiwa na timu ya wabunge kumi kutoka Bunge la Tanzania ambao ni marafiki na Bunge la China mara baada ya kuhitimisha ziara yake fupi ya kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Kampuni ya kutoka nchini kwake ya CCECC inayojenga Daraja la JP Magufuli na mradi wa Reli ya kisasa SGR kipande cha tano kutoka Isaka kuja Mwanza.

Balozi Chen amesema Makampuni 17 kutoka China yapo nchini kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni matokeo chanya ya mahusiano ya nchi mbili zenye mahusiano adhimu.

Ameongeza kuwa amefurahishwa kuona wataalamu kutoka Tanzania wanafanya kazi bega kwa bega kwenye mradi wa Daraja la JP Magufuli kwa lengo la kupata ujuzi zaidi ili kuja kuwa tegemeo katika miradi ijayo.

"Nchi yangu inanufaika sana kutokana na mahusiano mazuri tuliyonayo,tupo katika kujiimarisha na lugha ya kiswahili ili kufundisha kwenye vyuo vikuu vyetu na sehemu nyingine, watu kutoka China wapo hapa Tanzania kujipatia taaluma hiyo,"amesisitiza Balozi Chen.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa urafiki wa Wabunge baina ya Tanzania na China Mhe.Dkt.Charles Kimei,Mbunge wa Masasi mjini Mhe.Geofrey Mwambe amesema mradi wa Daraja la JP Magufuli na Reli ya kisasa utakuwa kitega uchumi cha uhakika kutokana na Mwanza kuwa na jirani na nchi za  maziwa makuu.

"Sina shaka yoyote na uwekezaji unaofanywa na China kwenye nchi yetu siku za nyuma nimekuwa Mtendaji Mkuu wa kituo cha uwekezaji nafahamu vizuri Tanzania tunavyonufaika,"Mhe.Mwambe.

Mradi wa Daraja la JP Magufuli uliyogharimu bilioni 716 unatarajia kukamilika Disemba mwakani wakati Reli ya kisasa SGR kipande cha kutoka Isaka hadi Mwanza wenye gharama ya zaidi ya Trilioni 3 utakamilika Mei mwakani.

Akiwa kwenye mradi wa SGR Wilayani Kishapu,Balozi Chen ametembelea kiwanda cha  kufyatua mataluma ya Reli na kuzungumza na wafanyakazi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti