• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

UJENZI WA MADARASA YA GHOROFA UBUNIFU MATUMIZI BORA YA ARDHI

Posted on: July 28th, 2025

Kutokana na ongezeko la watu na mahitaji ya ardhi kuwa makubwa katika maeneo mengi ya majiji nchini, Jiji la Mwanza limejipanga kufanya matumizi bora ya ardhi kwa kujenga madarasa kwa mfumo wa ghorofa ili kukidhi upatikanaji wa madarasa mengi katika eneo dogo.

Hayo yamebainika leo katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo aliyoifanya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda katika shule ya msingi ya mchepuo wa kiingereza na kukuta ujenzi wa madarasa 11 kwa mfumo wa ghorofa yanayogharimu zaidi ya Milioni 665 ambao umesaidia kupata madarasa mengi kwa eneo dogo.


Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mhe. Mkuu wa Mkoa amewapongeza Jiji la Mwanza kwa ubunifu huo na kubainisha kuwa kwa kufanya hivyo wataweza kupata madarasa mengi kwenda juu na kufuta msongamano wa wanafunzi kwenye madarasa bila kuanzisha ujenzi wa shule mpya pembezoni.

Amesema, maendeleo ya teknolojia yanashabihiana na uamuzi huo kwani unaruhusu uwekaji wa mifumo yote muhimu katika miundombinu kwa gharama nafuu katika eneo dogo kwa kuwa na madarasa, maabara na matundu ya vyoo katika eneo moja.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameipongeza Sahule ya sekondari Nsumba kwa kufunga mfumo wa nishati asilia kwa ajili ya kupikia uliogharimu Tshs. Milioni 7.8 ambao amesema utasaidia kupunguza gharama za uendeshaji na kupunguza uchafuzi wa mazingira ukilinganisha na matumizi ya kuni ya siku za nyuma.


Pamoja na kuwapongeza kutokana na kufaulisha katika madaraja ya 1-3 kwa wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita 2025 shuleni hapo, Mhe. Mtanda amekagua ufugaji wa samaki kwa njia ya kisasa ya vizimba unaofanywa na vikundi vya vijana 4 katika Mwalo wa Luchelele waliokopeshwa Milioni 360 na halmashauri hiyo.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa ameshuhudia jinsi halmashauri ya jiji ilivyoamua kutenga Tshs. Milioni 150 kusaidia ujenzi wa kituo cha polisi cha Nyegezi kinachojengwa kwa Tshs. Milioni 232, Milioni 708  zilizojenga miundombinu ya Kituo cha Afya Mkolani pamoja na 300 zilizonunua vifaa tiba ili kuwasogezea huduma wananchi wa maeneo hayo.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti