• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

UKITAKA KUIPENDA KAZI YAKO IKUBALI KWANZA - RC MTANDA

Posted on: July 29th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewaasa Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kuweka jitihada kwenye kazi zao kwa kuzikubali nafasi zao na kutekeleza majukumu yao kwa bidii ili waweze kuleta tija katika jamii wanazoziongoza.


Mhe. Mtanda ameyasema hayo leo tarehe 29 julai, 2025 wakati akiwahutubia Watendaji na Maafisa hao zaidi ya 300 kutoka katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Geita, Tabora na Kagera walioajiriwa

Kuanzia Julai, 2024.

“Kazi yako ukiipenda utaifanyia juhudi, na ukifanikiwa hayo basi utajikuta umejiendeleza kielimu, kuweka weledi na nidhamu, kwa ujumla kuishi ndani ya utumishi huo kizalendo.” Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka kutumia taaluma zao kuonesha tabia njema kwa jamii inayowazunguka na kuonesha uwezo kwenye kazi zao na staha ya maisha kwenye maeneo yao ya uongozi.

Kadhalika, amewataka kwenda kufanya maamuzi sahihi yanayozingatia sheria, kanunu na miongozo iliyowekwa katika sekta husika mathalani ardhi na sio kufanya uonevu kwa kundi moja au jingine kwani hali hiyo uharibu kazi.


Vilevile Mkuu wa Mkoa amewataka kwenda kuwaunganisha wananchi na sio kuwagawanya pia kuhakikisha wanawajengea ari ya kujitolea kwa serikali yao hususani kwenye uanzishwaji wa miradi ya maendeleo kama ujenzi wa madarasa, miradi ya maji na barabara.

Hata hivyo, amewataka kuishi kuendana na mazingira watakayoyakuta kwa wananchi wanaoishi nao katika maeneo yao ya kazi na kuwa wabunifu mathalani waonapo vyanzo vya mapato vipya na kuviwasilisha kwenye Halmashauri ili vipitiwe na kuingizwa katika maoteo ya kodi na ushuru.


Katika mafunzo hayo washiriki wamejengewa uelewa wa kina kuhusu muundo na majukumu yao ya kikazi, sera na sheria za Serikali, mbinu za kusimamia miradi ya maendeleo, namna ya kushughulikia kero za wananchi kwa wakati, pamoja na usimamizi bora wa rasilimali na mapato ya ndani.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti