• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Usalama wa Wananchi ni Kipaumbele changu- RC MAKALLA

Posted on: May 31st, 2023

*Usalama wa Wananchi ni Kipaumbele changu- RC MAKALLA*


*Aomba Ushirikiano kufanikisha Maendeleo mkoa wa Mwanza*


*Atangaza ratiba ya Usikilizaji Kero za wananchi Jimbo kwa Jimbo*


*Awataka watumishi kujibu kero za wananchi kwa wakati*


*Aagiza uimarishwaji wa Mapato ya ndani na Idara ya Ardhi isimame imara kutatua kero*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Amos Makalla amewataka viongozi wa wilaya ya Ilemela kusimamia masuala ya Usalama wa jamii ili wananchi wawe huru kufanya kazi za kujitafutia maendeleo.

CPA Makalla amebainisha hayo mchana wa leo Mei 31, 2023 kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela alipofika kujitambulisha kufuatia kuhamishiwa kwake na Mhe. Rais Mkoani Mwanza mapema mwezi huu.

"Watu wakikosa usalama watakosa amani ya kufanya mambo ya Maendeleo hivyo lazima tukumbushane umuhimu wa kuwa na amani kwenye maeneo yetu ili kuleta tumaini kwa wananchi kuwa wapo huru kujitafutia kipato." Amesema Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amesisitiza nidhamu ya kazi kwa watumishi ili wananchi wapate huduma bora na kuiamini serikali yao na kuondoa hofu na dukuduku kwa watumishi wa umma.

"Mkiwahudumia vyema mwananchi wataipenda Serikali na kinyume chake wataichukia hivyo tuepushe migogoro na migongano kwenye maeneo yenu ya kutolea huduma." CPA Makalla.

Vilevile, ameiagiza Halmashauri hiyo kusimamia kwa dhati ukusanyaji wa mapato ya ndani ili wawe na rasilimali za kutosha kutekeleza miradi mbalimbali kwa jamii na kwamba wote kwa pamoja ni lazima wadhibiti Mapato ya ndani na wajiwekee utaratibu wa kujibu Hoja za Ukaguzi kwa wakati.

"Hakikisheni fedha zote zinazokusanywa zinakwenda Benki ili tuweze kujihakikishia ukusanyaji mzuri na  kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza miradi mbalimbali na wabadhirifu wa fedha wajue kabisa kuwa tunawafuatilia" Amesisitiza.

Aidha, amewaagiza viongozi na watumishi kujibu kero za wananchi kwa wakati na kutosubiri ofisini bali wawafuate kwenye makazi yao na kwamba atafanya ziara ya kusikiliza kero za wananchi kwenye kila wilaya na atawapima wetakaobainika kuwa na kero nyingi.

"Nimekuja kuwasalimia na kujitambulisha kwenu hivyo naombeni sana ushirikiano wenu Viongozi, waheshimiwa Madiwani na watendaji wote tufanye kazi kwa pamoja ili kwenye mafanikio tuwe pamoja na kwenye Changamoto tuwe pamoja pia, hodi Mwanza." Mhe. Makalla.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masala amesema wilaya hiyo unaendelea kuboresha mazingira kwa kuwaletea huduma bora za Miundombinu, Elimu na Afya na kwamba makundi yote yanawezeshwa vema kupitia idara ya Maendeleo ya Jamii.

Aidha, amebainisha kuwa kwa Mwaka wa fedha inayoendelelea (2022/23) Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela imekadiria kukusanya Shilingi Bilioni 13 na hadi sasa wamekusanya zaidi ya bilioni 14 ambayo ni sawa na asilimia 109 na wanaendelea kutekeleza Miradi yenye thamani ya Bilioni 18.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti