• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

VIJANA WATAKIWA KUTUMIA VETA KUPATA UJUZI KWA GHARAMA NAFUU NA KUJIAJIRI

Posted on: February 28th, 2025

VIJANA WATAKIWA KUTUMIA VETA KUPATA UJUZI KWA GHARAMA NAFUU NA KUJIAJIRI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa wazazi nchini kupeleka vijana wao kupata elimu na mafunzo ya ufundi stadi katika vyuo vya VETA nchini ili wapate ujuzi kwa gharama nafuu na kuweza kujiajiri.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo  Februari 28, 2025 kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 30 ya utoaji huduma kwa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) yaliyofanyika katika viwanja vya chuo cha Mwanza.

"Leo tumeona katika maonesho ya vijana wetu jinsi gani wamepata ujuzi wa kutosha kwa fani mbalimbali jambo ambalo litawasaidia kujiajiri tena wamepata kwa gharama nafuu sana, natoa wito kwa vijana kutokaa vijiweni kuja kupata ujuzi." Mhe. Mtanda.

Akizungumzia darasa la madereva waliopewa ujuzi wa kuendesha magari na pikipiki amewataka vijana kufika kwenye vituo, kampasi na vyuo vya VETA nchini kwani kwa gharama nafuu ili kupata ujuzi utakao wasaidia kunusuru jamii kwa kuzuia ajali zinazoepukika.

"Zoezi la upandaji wa miti liwe endelevu kwenye taasisi na hata kwenye nyumba zetu kwani mabadiliko ya hali ya hewa yanategemea sana uhifadhi wa mazingira ili kutunza unyevunyevu na kusaidia hata kupatikana kwa maji kama kisima kilichokarabatiwa na VETA chenye umri mrefu." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Awali, Mkurugenzi wa VETA Kanda ya ziwa CPA. Janeth Nyoni amesema kwa kipindi cha miaka 30 chuo kimekua na kuongeza vyuo hadi 11 tofauti na 3 vilivyokuwepo awali na kwamba kwa mwaka 2025 kanda hiyo imedahili jumla ya wanafunzi 5000 katika fani za muda mrefu na mfupi.

"Katika kuadhimisha miaka 30 ya utoaji huduma tumefanya shughuli mbalimbali kama kutoa mafunzo ya udereva bila malipo, kupanda miti, wanafunzi kuchangia damu, kukarabati majengo kwenye haspitali pamoja na kisima cha maji kwa wananchi wa kata ya Buswelu wilayani Ilemela." CPA Nyoni.

Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) ilianzishwa mwaka 1995 na sheria ya bunge namba 1 ya 1994 ambapo ina jumla ya vyuo 80 nchini na 11 vikiwa katika kanda ya Ziwa ambapo mwaka 2026 vitaongezeka 14 na kufanya jumla ya vyuo 25.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti